LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 23, 2021

SPIKA NDUGAI: AZAKI TUMIENI TAFITI, TAKWIMU NZURI KUTATUA CHANGAMOTO KATIKA JAMII

SPIKA wa Bunge, Job Ndugai  akihutubia wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Wiki ya Azaki leo katika viwanja vya Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma.

Baadhi ya  wadau wa Asasi za kiraia  kiraia wakisikiliza kwa makini wakati Spika Ndugai akihutubia.



Na Richard Mwaikenda, Dodoma.

 SPIKA wa Bunge, Job Ndugai amezitaka Asasi  za kiraia  (Azaki)  kutumia tafiti  na takwimu vizuri  zitakazosaidia kutoa majawabu ya changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii ya watanzania.


Wito huo umetolewa na Spika Ndugai wakati wa ufunguzi wa Wiki ya AZAKI (2021) jijini Dodoma leo  ambapo amesema asasi hizo hazina budi kutafuta fedha ndani na nje ya nchi  kwa ajili ya kuleta tija  na vipaumbele vya taifa .


Aidha, Ndugai  amezitaka Asasi hizo kufanya kazi kwa weledi,uadilifu na uzalendo kwa maslahi mapana ya taifa.


Ndugai amezitaka asasi hizo kuwa na mwenendo wa kukosoa viongozi wa serikali lakini pia wana wajibu wa kuwapongeza hasa pale wanapofanya vizuri wanapotekeleza majukumu yao kwa ajili ya maslahi ya watanzania wote.

Kwa upande wake rais wa  Taasisi ya uwezeshaji asasi za kiraia (Foundation For Civil Societt- FCS) Dkt. Stigmata Tenga amesema ipo haja kwa bunge kuleta mabadiliko na  kupitia upya sheria, taratibu na miongozo ambayo inaziongoza asasi hizo  ili ziweze kushiriki vyema katika kutekeleza kazi zao na majukumu yao kwa maendeleo ya taifa.

Maonesho ya Wiki ya Azaki -2021) yanakwenda sambamba na kauli mbiu isemayo Azaki na Maendeleo.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages