LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 12, 2021

UPANDAJI MITI MSIUFANYE KAMA SHEREHE, BALI IWE KAZI ENDELEVU YA KUDUMU-RC MAHENGE+video


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge akiongoza kupanda miti eneo la Hospitali mpya ya Uhuru wilayani Chamwino  mkoani humo  siku ya maadhimisho ya Mapinduzi Tukufu ya Zanzibar Januari 12, 2021.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt Binilith Mahenge akizungumza  baada ya kazi ya kupanda miti kumalizika amapo aliwashukuru wote walioshiriki katika kazi hiyo muhimu ya utunzaji wa mazingira.

Mkuu wa Wilaya ya Chamwino, Vumilia Nyakoga  akishiriki kupanda miti eneo la Hospitali ya Uhuru.





Diwani wa Kata ya Buigiri ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, Kenneth Yindi akipanda mti katika eneo la Hospitali ya Uhuru ambayo ipo katika kata hiyo.



Dkt. Mahenge akjadiliana jambo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Maduka Kessy wakati wa kazi hiyo ya kupanda miti ikiendelea.



Mwanafunzi wa Udom, Mariam Hamza  akipanda mti.
Mwanafunzi Raphaela William wa UDOM, akiungana na wanafunzi wenzie wa Kitivo cha Elimu COED kupanda miti katika eneo hilo. 

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM, Chuo Kikuu cha Dodoma Kitivo cha Elimu, Godfrey Masele (kushoto) na Katibu Mkuu wa UVCCM wa  Kitivo hicho, Faris  Burhan  wakisaidiana kupanda mti  katika eneo hilo la Hospitali pamoja na wanafunzi wenzao 198.

Katibu Tawala Sekta za Uchumi wa Mkoa wa Dodoma, Aziza Mumba akipanda mti katika eneo hilo la Hospitali ya Uhuru.
Mwanafunzi Debora Adrian (kushoto) akisaidiana na mwenzie kupanda mti.
Mwanafunzi  Maida Abubakar akiwa makini kupanda mti.

 Na Richard Mwaikenda, CCM Blog, Dodoma

 

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge  ametoa mwito kwa wananchi kuacha tabia ya kulifanya suala la upandaji miti kama sherehe ama la msimu bali lifanywe kuwa endelevu na la kudumu.

 

Dkt. Mahenge ametoa kauli hiyo baada ya  kuongoza kazi ya upandaji miti  katika viunga vya Hospitali ya  Uhuru, wilayani Chamwino, Mkoa wa Dodoma leo.

 

“Nataka nitoe huu ujumbe kwamba,  wakati wote tusilichukulie hili zoezi la upandaji miti kama la kisherehe ama la misimu, nataka liwe endelevu, liwe la kila siku hasa wakati wa msimu wa masika,”alisema Dkt. Mahenge.

 

“Tusifanye kama kulipangia  tarehe fulani, mwezi Fulani au siku fulani , hapana ikifika wakati wa masika kila mmoja apande miti, kwani kazi ya kuokoa mazingira ni yetu sote,”amesisitiza Dkt. Mahenge.

 

Dkt. Mahenge amewashukuru watu wote walioshiriki katika kazi hiyo ya upandaji miti, wakiwemo wanafunzi 200 wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Kitivo cha Elimu (COED) ambao walimfuata ofisini kwake na kumuomba ashiriki nao kupanda miti eneo la Hospitali ya Uhuru, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli ya kuijenga hospitali hiyo kwa gharama ya sh. Bilioni 4.

 

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Chamwino, Vumilia Nyamoga, alimshukuru Mkuu wa Mkoa, Dkt. Mahenge kuhamasisha wanafunzi wa Udom kwenda kuungana na wananchi siku ya Sikukuu ya Mapinduzi Zanzibar, kupanda miti  kwa lengo la  kuthamini mchango mzuri wa Rais Magufuli wa kuwajengea wananchi Hospitali ya Uhuru.

 

Naye, Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Maduka Kessy  amesema kuwa siku hiyo ni njema  na yenye baraka kwa maana ya  kuadhimisha Sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar  sambamba na kupanda Zaidi ya miti 500  na kuifanya Dodoma kuwa ya kijani

.

 

Naye, Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Kitivo cha Elimu, Godfrey Masele, amesema kuwa wako tayari muda wowote kushiriki  katika mapinduzi makubwa  ya nchi yanayoendelea chini ya uongozi wa Rais John Magufuli na kwamba watakuwa tayari pia muda wote kushiriki kupanda miti kuifanya Dodoma kuwa ya kijani.

 

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Edson Sweti  aliwashukuru wote walioamua kuungana na wananchi wa Chamwino kwenda kupanda miti katika eneo hilo ambalo pia ni makazi ya Rais Magufuli na kuahidi kuitunza miti hiyo ili istawi vizuri.

 

Wakati huo huo, Zaidi ya wanafunzi 80 wa Udom baada ya kumaliza kupanda miti, walishiriki kuchangia damu katika Hospitali ya Uhuru ambayo imeanza kufanya kazi tangu Desemba 21, 2020.

 

Kabla ya kuanza kuchangia damu, wanafunzi hao walipatiwa elimu juu ya umuhimu wa suala hilo kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Damu Salama Hospitali ya Mkoa wa Dodoma,  Leah Kitundya.


Mdau karibu usikilize video hii ujue kilichozungumzwa...


IMEANDALIWA NA;
 RICHARD MWAIKENDA 
MHARIRI LOG YA TAIFA YA CCM
 0754264203

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages