LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 14, 2021

TUME YA TAIFA YA UMWAGILIAJI YANADI TOZO ZA UMWAGILIAJI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI.


kushoto Afisa Mazingira kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bi Christina Mwasaka akifafanua jambo kwenye kipeperushi kwa washiriki wa Ofisi hiyo katika Banda, ndani ya Maonesho yanayoendelea Mjini Moshi katika viwanja vya shule ya Msingi Mandela, kuelekekea maadhimisho ya siku ya Chakula Duniani.
 
Afisa Kilimo Mwandamizi kutoka Idara ya Uendeshaji Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Mohamed Mcheni, akifafanua Jambo kwa waandishi wa Habari hawapo katika picha, kwenye maonesho yanayoendelea mjini Moshi kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya chakula Duniani.

 Na Mwandishi Wetu –

Moshi

Ushiriki wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika maonesho
yanayofanyika mjini Moshi kuelekea maadhimisho ya siku ya chakula Duniani,
yameipa fursa ofisi hiyo kunadi sera zake kwa wananchi zinazowataka kisheria
wakulima, kulipa tozo za kilimo cha umwagiliaji.

Akizungumza na baadhi na wananchi waliotembelea banda la taasisi
hiyo, Bw. Mohamed Mcheni Afisa Kilimo Mwandamizi amesema kuwa, taratibu zote za
ukusanyaji wa ada umekamilika  na
kutangazwa katika gazeti la serikali, “Kwa mwaka huu wa fedha na miaka
inayoendelea tutaendelea kukusanya asilimia tano (5%), na kabla ya kulipa,
skimu inatakiwa isajiliwe.” Alisisitiza.

Aidha, Bw. Mcheni alisema kuwa Asilimia tano hiyo ni sawa na
wastani wa gunia moja kwa hekari kwa zao la mpunga na aliendelea kufafanua kuwa,
chama cha wakulima katika skimu za kilimo cha umwagiliaji zinatakiwa kulipa ada
ya usajili kiasi cha shilingi laki moja na elfu sabini na tano (175,000/-)
ambapo shilingi laki moja ni ada ya mwaka na shilingi elfu sitini ni ada ya
usajili, na shilingi elfu kumi na tano ni ada ya maombi ya usajili.

Alitoa wito kwa wakulima kulipa ada ya asilimia tano (5%) ya
wastani wa mavuno kwa msimu wa mwaka kwa hekari.

Maonesho kuelekea maadhimisho ya kilele cha siku ya Chakula
Duniani yenye kauli mbiu unayosema inayosema  “Zingatia Uzalishaji na Mazingira Endelevu kwa
lishe na Maisha Bora” yanafanyika Mjini Moshi mkoani Kilimanjaro katika kiwanja
cha shule ya msingi Mandela.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages