Mar 2, 2025

MWAMUZI ARAJIGA ATEULIWA NA FIFA KUCHEZESHA BOTWANA, ALGERIA


 WAAMUZI wa Tanzania Ahmed Arajiga, Kassim Mpanga, Said Hamdani na Salum Nasir wameteuliwa na na Shirikisho la soka Duniani (FIFA) kuchezesha mchezo wa Kundi G wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2026 kati ya wenyeji Botswana dhidi ya Algeria utakaopigwa Mjini Francistown Nchini Botswana Machi 21, 2025.

Algeria na Msumbiji wapo kileleni mwa Kundi G wakiwa na pointi 9 kila mmoja wakifuatiwa na Botswana, Guinea, na Uganda wenye pointi 6 kila mmoja huku Somalia ikiburuza mkia bila pointi yoyote

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Pages