Alhaj Dk. Mzimbiri kwa sasa ndiye Mkuu wa Kitengo cha Dharura na Ajali (Emergency). Pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa kliniki ya kibingwa ya THE CURE iliyopo Upanga mtaa wa Mindu na Maliki jijini Dar es salaam.
Amesomea taaluma yake nchini China, India na Marekani na amekuwa akiendesha vipindi mbalimbali vya afya katika vyombo vya nchini kama Azam Tv na vya kimataifa kama BBC na Umoja wa Mataifa UN Tv.
Pia Alhaj Dk. Mzimbiri ni mshindi wa tuzo za Tafiti za Kansa zilizotolewa na Waziri wa Afya Jenista Mhagama katika Hospital ya Shifaa iliyopo jijini Dar es salaam. kwa upande wa CCM, ni Mjumbe wa CCM katika tawi la Tambaza, Kata ya Upanga Magharibi jijini Dar es salaam.Alhaj Dk. Mzimbiri akikabidhi fomu yake kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Lushoto, Miriam Kaaya jana. Katikati ni Baba yake Mzazi Idriss Abushehe Musa Mimbiri. Alhaj Dk. Mzimbiri akiwa na fomu yake kabla ya kuirejesha jana.
Waziri wa Afya Jenista Mhagama akimkabidhi tuzo Alhaj Dk Mzimbiri ambaye aliibuka mshindi wa tuzo za Tafiti za Kansa. hafla hiyo ilifanyika Hospital ya Shifaa iliyopo jijini Dar es salaam.
Chini ni picha mbalimbali Alhaj Dk. Mzimbiri akiendesha vipindi
mbalimbali vya afya katika vyombo vya Azam Tv, BBC na Umoja wa Mataifa UN Tv.
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇