LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 21, 2022

WATAALAM WA AFYA NCHINI WAPATIWA MAFUNZO YA KIMATAIFAA JINSI YA KUFANYA KIPIMO CHA MOYO KWA KUTUMIA MASHINE YA ECHOCARDIOGRAM (ECHO)

  Mkuu wa Kitengo cha Mafunzo na utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea namna mafunzo ya Echo yatakavyofanyika kwa washiriki wa mafunzo ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanya kazi kwakutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) yanayoendelea katika Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA) 
Mbunge wa viti Maalum Mhe. Dkt. Alice Kaijage akielezea ujuzi atakaoupata katika mafunzo ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) yatakavyomsaidia katika taaluma yake wakati wa mafunzo hayo ya siku mbili yanayoendelea katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo Jijini Dar es Salaam.
   Mbunge wa viti Maalum Mhe. Dkt. Alice Kaijage akielezea ujuzi atakaoupata katika mafunzo ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) yatakavyomsaidia katika taaluma yake wakati wa mafunzo hayo ya siku mbili yanayoendelea katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo Jijini Dar es Salaam.
   Daktari bingwa wa magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Piedmont Health iliyopo Atlanta Georgia nchini Marekali Dkt. Mani Vannan akiwafundisha watalaam wa afya kutoka hospitali mbalimbali nchini namna ya kupima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) wakati wa mafunzo hayo yanayoendelea katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Jijini Dar es Salaam.
   Wataalam wa afya kutoka hospitali mbalimbali nchini wakifuatilia mafunzo yaliyokuwa yakitolewa na mkufunzi kutoka Taasisi ya Piedmont Health iliyopo Atlanta Georgia nchini Marekali Dkt. Mani Vannan ya namna ya kupima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) wakati wa mafunzo hayo yanayoendelea katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Jijini Dar es Salaam.
Wataalam wa afya kutoka hospitali mbalimbali nchini wakifuatilia mafunzo yaliyokuwa yakitolewa na mkufunzi kutoka Taasisi ya Piedmont Health iliyopo Atlanta Georgia nchini Marekali Dkt. Mani Vannan ya namna ya kupima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) wakati wa mafunzo hayo yanayoendelea katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) yanayoendelea katika Taasisi hiyo Jijini Dar Es Salaam. Mafunzo hayo yaliyoudhuriwa na wataalam wa afya zaidi ya 100 yamefanyika kwa mara ya kwanza hapa nchini.


Na: Genofeva Matemu – Dar es Salaam

19/08/2022 Wataalam wa afya zaidi ya 100 kutoka hospitali binafsi na hospitali za umma wameshiriki mafunzo yakimataifa ya siku mbili ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) ambayo yamefanyika kwa mara ya kwanza hapa nchini.

Akizungumza na waandhishi wa Habari wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo leo Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi alisema kuwa mafunzo hayo yanatolewa na wakufunzi na wabobezi wakuu wa magonjwa ya moyo kutoka nchini Marekani.

Prof. Janabi alisema kuwa lengo la mafunzo hayo nikuongeza ujuzi kwa wataalam wa afya ili kusaidia na kupunguza wagonjwa ambao wanaingia gharama kutoka mikoani kwenda JKCI kwa ajili ya kufanyiwa kipimo cha Echo kwani wakiweza kuwagundua katika maeneo yao ya kazi wataweza kuchagua wagonjwa wanaohitaji kufanyiwa matibabu zaidi na kuwatuma JKCI.

“Tumekua tukifanya mafunzo kama hayo huko nyuma lakini kwa kutumia wataalamu wetu wa ndani ndio maana leo tunasema haya ni mafunzo yetu ya kwanza yakimataifa kwasababu tuna wabobezi na wataalam zaidi katika uchunguzi wa jinsi moyo unavyofanya kazi (ECHO) kutoka nchini Marekani”,

“Kwetu sisi wataalam wakutoa huduma za matibabu ya moyo, hatuwezi kufanya upasuaji wa aina yoyote bila kufanya kipimo cha Echo hivyo ujuzi tutakaoupata hapa utasaidia zaidi kuboresha huduma zetu na  kuchagua wagonjwa wapi waende kwenye upasuaji na wangapi wanaweza kutumia dawa bila ya kufanyiwa upasuaji”, aliseama Prof. Janabi

Prof. Janabi alisema kuwa mafunzo ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanyakazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) yataendelea kutolewa kila mwaka kwa wataalam wote wa afya bila kubagua waliopo katika hospitali za umma na zile za binafsi ili kujifundisha mbinu mpya za kugundua matatizo ya moyo awali kabla ya tatizo kuwa kubwa.

Mshiriki wa mafunzo hayo ambaye ni Mbunge wa viti maalum Mhe. Dkt. Alice Kaijage alisema kuwa ameshiriki mafunzo ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) ili aweze kupata mbinu mpya na zakisasa katika kutoa huduma za matibabu ya moyo.

“Nikiwa bungeni tuna kituo cha afya hivyo kwanjia moja ama nyingine naweza kusaidiana na wenzangu kama mtaalamu kupima moyo unavyofanya kazi kwa wagonjwa wanaofika katika kituo hicho lakini pia kupitia taaluma yangu natakiwa kuongeza ujuzi ili niweze kuendana na maendeleo ya sayansi na teknolojia”

Kwa upande wake Mkufunzi kutoka Taasisi ya Piedmont Health iliyopo Atlanta Georgia nchini Marekali Dkt. Mani Vannan alisema kuwa anaamini katika mafunzo ya mara kwa mara katika taaluma ya afya na nimoja ya matamanio yake kuona wataalam wa afya wanashiriki mafunzo ya kuongeza taaluma zao kila wanapopata fursa.

“Naamini Taasisi hii inamisingi mizuri katika taaluma ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO), madhumuni ya mafunzo haya nikuifanya nchi hii kuwa kituo cha ubora katika utoaji wa huduma za kibingwa za vipimo na matibabu ya moyo”, alisema Dkt. Mani

Naye Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Tiba Shirikishi katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delila Kimambo alisema kuwa kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanyakazi ni moja ya huduma za tiba shirikishi ambayo nimuhimu kwa mtaalam wa afya kujua matatizo aliyonayo mgonjwa na kumpa mwelekeo wa huduma gani mgonjwa anastahili kupewa.

“Mgonjwa yeyote wa moyo nilazima afanyiwe kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (ECHO), ni kipimo muhimu ambacho wataalam waliopo hapa leo wanapaswa kukifahamu kwa undani zaidi ndio maana tumeandaa mafunzo haya ili tuwakumbushe na kuwafundisha waweze kutoa huduma hiyo katika ubora zaidi”,

“Unapofanya kipimo cha Echo vyema zaidi unamsaidia mgonjwa kupata huduma bora zaidi, kumpa taarifa sahihi itakayomsaidia katika matibabu yake pamoja na kujua tatizo lake kama linahitaji dawa ama upasuaji”, alisema Dkt. Delila

 
 

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages