Meneja
Urasimishaji Ardhi Vijijini wa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na
Biashara za Wanyonge Tanzania (Mkurabita), Anthony Temu akielezea
umuhimu wa wananchi wa Kijiji cha Mkundi, Kata ya Dumila, wilayani
Kilosa, Morogoro kushiriki kazi ya kupima mashamba yao ya kilimo cha
miwa ili wapate hati miliki za kimila.
Temu
aliwaeleza kuwa wakipata hati miliki za kimila wataweza kuzitumia kuweka
kama dhamana kukopa fedha benki na taasisi zingine za fedha
zitakazowasaidia kupanua kilimo cha miwa na kuboresha miradi yao mingine.
Aliyazungumza
hayo katika kikao cha Halmashauri ya Kijiji cha Mkundi na wakati wa
Mkutano wa hadhara wa wananchi wa Kijiji hicho, ambapo waliukubali
mpango huo kwa kauli moja na kuishukuru Mkurabita kwa kuwakumbuka na
kuuomba uongozi wa Mkurabita kupima pia mashamba mengine zaidi.
Wajumbe wa Halmahauri ya Kijiji wakiwa meza kuu pamoja na uongozi wa Mkurabita na maafisa wa Halmashauri ya wilaya ya Kilosa wakati wa mkutano wa hadhara wa kijiji.
Sehemu ya wananchi wakiwa kwenye mkutano wa hadhara.
Viongozi wa Kijiji wakiangali ramani ya Kijiji ch Mkundi katika hati waliyokabidhiwa kutoka wilayani.
Wananchi wakisikiliza kwa makini wakati wa mkutano wa hadhara.
Mwenyekiti wa Kijiji ch Mkundi, Boniventure Flawan akiwahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi katika kazi ya upimaji wa ardhi.
Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Mkundi, Martine Mshanga akifafanua jambo wakati wa mkutano wa hadhara.
Mdau Nakuomba uendelee kusikiliza clip hii ya video ujue yaliyojiri kwenye mkutano huo wa kijiji....
Imeandaliwa na Richard Mwaikenda
Mhariri Blog ya Taifa ya CCM.
0754264203
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇