LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

May 11, 2021

RAIS SAMIA ATEUA MAJAJI 7 WA MAHAKAMA YA RUFANI NA 21 WA MAHAKAMA KUU, LEO

Rais Samia


Ikulu, Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Majaji saba wa Mahakama ya Rufani, 21 wa Mahakama Kuu na ku muongezea muda Jaji mmoja wa Mahakama ya Rufani.


Taarifa iliyotolewa na Ikulu jijini Dar es Salaam, imewataja Majaji wa Mahakama ya Rufani walioteuliwa kuwa ni; Patricia Saleh Fikirini ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Jaji Mfawidhi – Divisheni ya Biashara, Mahakama Kuu ya Tanzania (Dar es Salaam), Penterine M. Kente ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania (Iringa).


Dk. Paul Faustine Kihwelo ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama, Lushoto Mkoani Tanga, Lucia Gamuya Kairo ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania (Bukoba).


Lilian Leonard Mashaka ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Jaji Mfawidhi – Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Mahakama Kuu ya Tanzania (Dar es Salaam), Issa John Maige ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Jaji Mfawidhi – Divisheni ya Ardhi, Mahakama Kuu ya Tanzania (Dar es Salaam).


Abraham Mwampashi ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar.

Uteuzi wa Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Patricia Saleh Fikirini ulianza tarehe 05 Mei, 2021, wakati uteuzi wa Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya Rufani wengine umeanza tarehe 11 Mei, 2021.

Aidha, Mhe. Rais Samia amemuongeza muda wa miaka 2 Mhe. Sivangilwa Sikalalilwa Mwangesi wa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kuanzia tarehe 15 Februari, 2021.


Majaji wa Mahakama Kuu walioteuliwa ni;

Katarina Tengia Revocati ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe.


Biswalo Eutropius Mganga ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Zahra Abdallah Maruma ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Naibu Msajili, Mahakama ya Rufani Tanzania na Mkuu wa Kitengo cha Maboresho ya Mahakama (JDU) katika Wizara ya Katiba na Sheria.


Devotha C. Kamuzora ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Naibu Msajili wa Baraza la Rufani la Kodi (TRAT), Dar es Salaam, Chaba Messe John ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Naibu Msajili Mfawidhi, Masjala Kuu ya Mahakama Kuu Dar es Salaam.


Lilian Jonas Itemba ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Wakili wa Serikali Mwandamizi katika Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Awamu Ahmada Mbagwa ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Wakili wa Serikali Mwandamizi, Ofisi ya Mashtaka Dodoma.


Mhe. Ayoub Yusuf Mwenda ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Mkurugenzi Msaidizi, Ofisi ya Mwendesha Mashtaka, Nyigulile Robert Mwaseba ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania (Dar es Salaam).


John Francis Nkwabi ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu (Arusha),

Safina Henry Simfukwe ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Ardhi.


David Patrick Nguyale ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Frank Habibu Mahimbali ambaye kabla uteuzi huu alikuwa Naibu Msajili Mfawidhi, Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mwanza.


James Karayemaha ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Emmanuel Loitare Ngigwana ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Naibu Msajili Baraza la Kodi, 

Abdi Kagomba ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Meneja wa Huduma za Sheria wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA).


Arafa Mpinga Msafiri ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Msaidizi wa Katibu wa Baraza la Mawaziri, Katiba na Sheria, Ofisi ya Rais Ikulu, Dkt. Ubena John ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Mhadhiri na Mkuu wa Kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu Mzumbe, 

Dk. Eliamini Isaya Laltaika ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Tumaini.


Dk. Theodora Mwenegoha ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mwanabaraka Saleh Mnyukwa ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Mhadhiri wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama.


Uteuzi wa Majaji wa Mahakama Kuu umeanza leo tarehe 11 Mei, 2021.


Tarehe ya kuapishwa kwa Majaji wa Mahakama ya Rufani na Majaji wa Mahakama Kuu walioteuliwa katika uteuzi huu itatangazwa baadaye.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages