LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

May 13, 2020

DK KABATI MBUNGE WA KUIGWA MAPAMBANO DHIDI YA CORONA


Mbunge Dk. Ritha Kabati

                        Na Richard Mwaikenda
MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa, Dk. Ritha Kabati amechapisha kitabu cha kurasa 15 kinachoelezea  alivyoshiriki katika kampeni ya kuelimisha wananchi jinsi ya kukabiliana na janga la Corona.

Kampeni hiyo ameifanya katika vijiji mbalimbali vilivyopo katika wilaya tatu za mkoa wa Iringa, ambazo ni Mufindi, Kilolo na Iringa.

Katika kuhakikisha Serikali inafanikisha azma yake ya kukabiliana na ugonjwa wa  homa kali ya mapafu  Covid19 unaotokana na virusi vya Corona, ulioenea Duniani kote. Dk. Kabati, ameamua kufanya  ziara ya mkoa mzima ili kufikisha ujumbe wa namna bora ya kujihadhari na usambazaji wa ugonjwa huo.
Alianza ziara yake katika Wilaya ya Iringa Vijijini, ambapo alitoa elimu ya nyumba kwa nyumba kuona namna wanavyochukua tahadhari na wanavyoutafsiri ugonjwa huo. Aliweza kuzifikia kata zote za wilaya hiyo na kuonana na wananchi pamoja na viongozi wa serikali, CCM, UWT na Jumuia zake zote.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Vijijini, Dk. Kabati, alitembelea pia Kituo cha  Afya cha Ipamba ili kujua utayari wao wa kugundua  watu kwenye kuhisiwa  kupata maambukizi ya ugonjwa huo hatari.

Katika Kituo hicho, Dk. Kabati alibaini uwepo wa utaratibu maalumu wa kuwapima joto watu wote  wanaoingia hapo kwa kuwa na kifaa maalumu  cha kupimia joto. Uwepo wa chumba maalumu kilichotengwa kwa watakaohisiwa. 

Wameagiza vifaa maalumu  kwa ajili ya wauguzi kujikinga wakati wa kutoa tiba. Utoaji elimu kuhusu Corona ulikuwa unaendelea.

Katika Wilaya ya Kilolo, Mbunge huyo ambaye ni mfano wa kuigwa kwa uchapakazi, alijikita kutembelea katika maeneo ya biashara na yenye mikusanyiko ya watu, ambapo alibaini baadhi ya maeneo wakiwa wamechukua tahadhari kwa kuweka maji tiririka na vitakasa mikono. Maneo hayo ni:Kata ya Ilula, Nyalumbu, Ruaha Mbuyuni, Lugalo na Mtitu.
Pia, aliyabaini maeneo yanayohitaji kutolewa elimu zaidi ambayo ni: Kata ya Kimara, Idete, Nga’ng’ange, Dabaga na nyinginezo kutoka Kilolo Milimani. Pia alishauri elimu itolewe zaidi katika maeneo ya usafiri wa Daladala, Bodaboda na Bajaji ikiwa na uwekaji wa maji tiririka na vitakasa mikono.

Alizungumza na viongozi mbalimbali wakiwemo wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), juu ya kuendelea kutoa elimu na kuwa mfano wa kuigwa kwa jamii inayowazunguka, ambapo pia aliwawezesha kiasi cha fedha ili kununua vifaa vya kujikinga na maambukizi ya Corona.
Katika Wilaya ya Iringa Mjini, Dk. Kabati, alianza kwa kuitembelea  Hospitali ya Mkoa wa Iringa, ambapo alisikitishwa  kuona kutokuwepo utayari wa vipima joto vya kuwatambua wanaohisiwa kuwa na Corona, jambo ambalo ni hatari hasa kwa hospitali hiyo inayohudumia watu wengi.

Pia, Dk. Kabati alipata wasaa wa kutembelea Bohari ya Madawa ya Mkoa wa Iringa na Nyanda za Juu Kusini kuona upatikanaji wa  vifaa vya Corona, ambapo alibaini ukosefu wa  vifaa muhimu katika kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa huo hatari.
Katika Wilaya ya Mufindi, Mbunge huyo alijikita kutembelea maeneo ya biashara na vituo vya afya kuona namna wanavyochukua tahadhari ya ugonjwa huo, ambapo katika Mnada wa Kata ya Maduma, alibaini asilimia ya wananchi waliokuwepo, kutokuwa na wasiwasi wa ugongwa huo licha ya kuwa na elimu kiasi ya kuwepo ugonjwa huo wa Covid 19 nchini.
Viongozi wa Kata hiyo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) aliozungumza nao juu ya suala hilo, waliahidi kushiriki kutoa elimu ya kujikinga na maambukizi  ya ugonjwa huo licha kuwa na changamoto zifuatazo: Ukosefu wa vifaa vya kujikinga, uhitaji wa watalaamu zaidi wa kutoa elimu, na uhitaji wa viongozi wa juu wa serikali wanaoweza kupita katika maeneo ya kutoa elimu.

Alifanya ziara katika Kituo cha Afya cha Ifwagi kinachohudumia kata nyingi tofauti na uwezo wake. Ambapo hata hivyo alikuta tayari wameshaweka maji tiririka na vitakasa mikono, kimeendelea kuwatumia watalaamu wake kutoa elimu juu ya ugonjwa huo, kimetenga chumba maalumu cha kuwatenga wagonjwa wanaoshukiwa kuwa na virusi vya Corona.
Amezitaja baadhi ya changamoto alizozikuta kituoni hapo kuwa ni; Chumba cha kuwatenga wagongwa  ni kidogo na kina kitanda kimoja, Kituo hakina vifaa vya kujikinga kwa wauguzi, ikiwemo barakoa, nguo maalumu za kujikinga na maambukizi, vipimo vya kutambua joto kwa haraka bila ya kugusana, pia kituo hakina vipeperushi kwa ajili ya kutoa elimu zaidi ya ugonjwa.

Dk. Kabati amezitaja baadhi ya changamoto alizozibaini kwa ujumla wakati wa ziara zake kuwa ni; Kutokuwepo kwa vitakasa mikono katika maeneo mengi, bado kuna maeneo yenye mikusanyiko isiyo ya lazima, baadhi ya watu hawana elimu ya  kujikinga dhidi ya corona, bado wapo wakazi wa maeneo wenye imani potofu kuwa ugonjwa huo hautaweza kusambaa vijijini, vituo vingi vya afya havina vifaa vya wauguzi  kujikinga na maambukizi ya Corona.

Baada ya kuona changamoto hizo, Mbunge huyo alichukua hatua za kuwashauri  viongozi wa Kata husika kutoa elimu kwa wananchi juu ya kukabiliana na ugonjwa huo, aliwashauri watalaamu wa afya kuta elimu ya kitalaamu ili kuondokana na dhana potofu zinazosambazwa mitaani.

Pia, aliwashauri  Watendaji wa Serikali kufunga biashara za wafanyabiashara  wasiochukua tahadhari ya maambukizi ya Corona, aliagiza vifaa katika Bohari ya Dawa Mkoa wa Iringa ili kupatiwa wauguzi wa Kituo cha Afya Ifwagi kwa ajili ya kujilinda. Alikabidhi fedha  kwa viongozi wa kata alizozitembelea kwa ajili ya kununulia vifaa kinga.

Ili kuepukana na maambukizi ya Corona, Dk. Kabati amewataka wananchi kuepuka kuingia kwenye misongamano, kukaa umbali wa mita moja na mtu mwingine, kunawa maji tiririka kwa sabuni pamoja na kutumia vitakasa mikono, usiguse macho,pua na midomo kama hujanawa, kuvaa barakoa, epuka kuwa karibu sana na mgonjwa, safisa mara kwa mara vitu unavyovigusa kama vile vikombe, meza, dawati pamoja na simu yako.

Amemalizia kwa kutoa ushauri kwa Serikali za Vijiji kuchukua hatua dhidi ya wafanyabiashara na wakazi  wasiochukua hatua za kujihadhari na maambukizi ya
maeneo ya vituo vya usafiri kama vile, mabasi, daladala, bodaboda na bajaji yawe na maji ya kunawa pamoja na vitakasa mikono. Masoko na minada isiyochukua tahadhari ya maambukizi ya Corona yatizamwe upya namna ya utoaji bora wa huduma na viongozi wa Dini wapatiwe vipeperushi ili kutoa elimu zaidi kwa waumini wao. 










No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages