LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 15, 2020

MASHAMBULIO YA KUNDI LA KIGAIDI LA AL-SHABAB WALIMU KENYA WAENDELEA KUHOFIA USALAMA WAO

Jan 15, 2020 12:42 UTC
  • Walimu nchini Kenya waingiwa na kiwewe cha mashambulio ya wanamgambo wa al-ShababWalimu nchini Kenya wanaofanya kazi katika eneo la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo wanaendelea kuhofia usalama wao kutokana na kuweko vitisho vya mashambulio ya kundi la kigaidi la al-Shabab.
Wasiwasi wa walimu huo umekuja siku chache baada ya watu wanaosadikiwa kuwa wanachama wa kundi la kigaidi la al-Shabab kuwashambulia na kuwauwa wenzao wanne na kuwajeruhi wengine kadhaa mwishoni mwa wiki iliyopita katika Kaunti ya Garissa.
Chama cha Walimu nchini Kenya (KNUT) nacho kimetoa wito kikiitaka serikali ya Kenya kuchukua hatua madhubuti ili kuwahakikishia usalama wa walimu hao.
Shambulizi lililofanywa na wanagmabo wa al-Shabab dhidi ya Shule ya Msingi ya  Kamuthe katika Kaunti ya Garissa, limezua hasira na wasiwasi mkubwa miongoni mwa walimu katika eneo hilo linalopakana na nchi ya Somalia. Gavana wa Garissa, Ali Korane amevitaka vyombo vya usalama kuimarisha ulinzi katika eneo hilo.
Shambulio la al-Shabab katika Chuo Kikuu cha Garissa  Apili Pili, 2015
Kundi la kigaidi la al-Shabab ni tawi la mtandao wa kigaidi al-Qaeda nchini Somalia na limefanya mashambulizi mengi  ya kigaidi katika nchi jirani ya Kenya likilenga idara za serikali, askari, magari ya abiria na mahoteli.
Mauaji ya kigaidi katika Chuo Kikuu cha Garissa, ni shambulio kubwa zaidi kuwahi kufanywa nchini Kenya na wanamgambo hao tangu mwaka 1998. Watu 148 waliuwa wengi wao wakiwa wanafunzi wa chuo hicho katika shambulio hilo la kivamizi la al-Shabab la Aprili Pili mwaka 2015

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages