Mbunge wa Mbeya Mjini ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya, Patrick Mwalunenge ameiomba serikali kuuruhusu mkoa huo kukopa fedha za kujenga Km 100 za Jiji la Mbeya na kwamba uwezo wa kulipa deni hilo wanao. bungeni Dodoma Aprili 14, 2026. Pia Mwalunenge ameiomba serikali kuupatia mkoa huo fedha zitakazosaidia kukarabati masoko mbalimbali ya Jiji hilo ambayo yamechakaa.
Aidha ameishauri serikali kujenga Mbeya kongani ya viwanda vya kuongeza thamani ya mazao, pamoja na kujenga ukumbi mkubwa wa kisasa wa mikutano. Ameyasema hayo alipokuwa akichangia mjadala wa hotuba ya Waziri Mkuu.
No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇