Marehemu
alikuwa mchungaji mwaminifu na kiongozi mwenye hekima na busara,
aliyelitumikia Kanisa na Taifa kwa uaminifu mkubwa, akiacha alama
isiyofutika katika mioyo ya wengi.
Kwa
niaba yangu binafsi na kwa niaba ya Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa
Mazingira (TRAMEPRO), ninawasilisha salamu za rambirambi kwa Kanisa
Katoliki, familia ya marehemu, waumini wote, na Watanzania wote
walioguswa na msiba huu mkubwa katika Kanisa na Taifa letu.
Tunamwomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi, apumzike kwa amani ya milele.
“Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo alikuwa kama sisi, nasi tutakuwa kama yeye; hivyo tujiandae.”
Imetolewa na:
Boniventura Mwalongo
Katibu Mkuu – TRAMEPRO
Tarehe: 24 Februari 2026



No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇