Apr 14, 2025

MABALOZI WAUNGA MKONO KUTANGAZA VIVUTIO VYA TANZANIA

 

“Nimetembelea nchi nyingi zenye wanyama, lakini Tanzania ina upekee wa asili – kuanzia bioanuai ya wanyama, wadudu hadi mimea. Nimevutiwa zaidi na mazingira ya asili,” amesema na kuongeza:

“Naishauri Tanzania kuongeza nguvu katika kutangaza vivutio hivi. Mkifanikiwa, mnaweza kuwa nchi iliyoendelea kwa kutegemea utalii pekee. Uzuri ni kwamba mimi naenda kuanza kuwatangaza – na naahidi wengi watakuja.”

Naye Mkuu wa Kitengo cha Miamala ya Kibenki kutoka NMB, Bi. Linda Teggisa, amesema lengo la kuwakutanisha mabalozi na wakuu wa misheni za kidiplomasia pamoja na wawakilishi wa taasisi za kimataifa ni kuwaeleza kuhusu masuluhisho ya kifedha – hususan ya kidijitali – ambayo NMB inatoa kwa sekta ya utalii.

“Tumewaeleza kuhusu masuluhisho yenye mlengo wa kujenga uwezo wa kifedha kwa wawekezaji – kama mikopo ya kununua magari na vifaa vingine muhimu kwa shughuli za utalii.”

Ameongeza kuwa kwa sasa, NMB inawekeza zaidi katika huduma za kidigitali ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya kiteknolojia.

“Zaidi ya asilimia 94 ya miamala yetu sasa inafanyika kidigitali. Tunawekeza nguvu zaidi huko kuhakikisha hakuna mteja anakwama kupata huduma – popote alipo ndani au nje ya nchi,” amesema.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa, amesema wizara imeandaa ziara hiyo kwa lengo la kuwapa fursa wadau wa kidiplomasia kuona vivutio vya Tanzania kama njia ya kukuza mahusiano na utalii.

“Utalii unazidi kuwa uti wa mgongo wa uchumi wetu. Kwa sasa unachangia asilimia 25 ya pato la taifa, na tunalenga kuongeza hadi kufikia nusu ya mapato yote, kwa kufikia zaidi ya watalii milioni saba kwa mwaka.”

Ameeleza kuwa katika awamu ya kwanza ya ziara hiyo, wameshiriki wajumbe 25 kutoka nchi mbalimbali, na lengo ni kuwashirikisha wajumbe wote 93 walioko na wanaoshirikiana na Tanzania.

“Wamepata nafasi ya kutembelea Serengeti, Ngorongoro, na sasa wanakwenda Zanzibar kushuhudia vivutio vilivyopo huko pia. Tunaamini watakuwa mabalozi wazuri wa nchi yetu,” amesema Balozi Mussa.





 

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Pages