Mar 27, 2025

SH. MIL. 374 ZATUMIKA KUFUNGA INTANETI YA BURE MAENEO YA WAZI - UCSAF



 Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), umetumia  Sh.mil. 374 kufunga mtandao wa bure wa Intaneti maeneo ya wazi nchini  kwa lengo la kuongeza wigo wa matumizi ya intaneti.


Hilo limeelezwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa UCSAF, Mhandisi Peter Mwasalyanda wakati akizungumza na Waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa Idara ya Habat MAELEZO jijini Dodoma Machi 27, 2025, kuhusu mafanikio na mwelekeo wa mfuko huo kwa Kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita inaoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan .


"UCSAF imefunga Public Free WiFi katika maeneo 7 na mengine  17 katika Viwanja vya maonesho ya Sabasaba Dar es Salaam, ili kuongeza wigo wa Intaneti," amesema Mwasalyanda.


 Ametaja maeneo waliyofunga  mtandao huo kuwa ni;

  i.        Chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Lungemba (Mafinga)

 ii.        Nyerere Square (Dodoma)

iii.        Ndaki ya Habari na Elimu Angavu (CIVE) Chuo Kikuu cha Dodoma

 iv.        Soko la Tabora (Tabora)

 v.        Kiembe Samaki (Unguja) na

 vi.        Soko la Buhongwa (Mwanza).

vii.        Maeneo Mengine 17 katika Viwanja vya maonyesho ya Sabasaba


Aidha,Mwasalyanda amesema kuwa watafanya utafiti vijijini kubaini maeneo yenye mikusanyiko ya watu wengi kama vile kwenye masoko na kuweka mtandao wa Intaneti.

Afisa Mtendaji Mkuu wa UCSAF, Mhandisi Peter Mwasalyanda wakati akizungumza na Waandishi wa habari katika mkutano huo.

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari MAELEZO, Rodney Thadeus akitoa neno la kuhitimisha mkutano huo.
Waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo.




Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari MAELEZO, Rodney Thadeus akimsindikiza Afisa Mtendaji Mkuu wa UCSAF, Mwasalyanda.

IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
MHARIRI
BLOG YA TAIFA YA CCM
0754264203





No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Pages