LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 25, 2024

CHAMA CHA KIKOMUNISTI CHA VIETNAM (CPV) CHASEMA NCHI HIYO INAIPA KIPAUMBELE CHA KIPEE TANZANIA AFRIKA

CCM's Official Blog, CCM Lumumba, Dar es Salaam
Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam (CPV) kimesema nchi hiyo inaipa Tanzania kipaumbelea cha kipekee katika kujenga na kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia, kisiasa na kiuchumi katika nchi za Afrika.

 

Kimesema kinafanya hivyo kutokana na uhusiano baina ya nchi hizo uliojengeka kiuhalisia kwa miaka 60 sasa.

Hayo yamesemwa leo na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho (CPV), Phan Dinh Trac, wakati ujumbe wa viongozi waandamizi 12 wa CPV aliouongoza, walipotembelea Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam, na kufanya mazungumzo na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara John Mongella.

Amesema kutokana na sababu hiyo Vietnam itaendelea kushirikiana na kuimarisha uhusiano wake na Tanzania, na kuiomba CCM na Seikali yake kuwa kiunganishi na kutoa fursa kwa Wa-Vietnam kuwekeza nchini ikiwa njia mojawapo ya kudumisha ushirikiano na mahusiano yaliyopo.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara John Mongella ameishukuru Vietnam na Chama cha CPV kwa kuiona Tanzania kuwa nchi ya kipekee katika mahusiano kwenye nyanja mbalimbali, na kuahidi kwamba CCM chini ya Mwenyekiti wake Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kitaendelea kudumisha uhusiano uliopo baina ya nchi hizo mbili.

Ameipongeza Vietnam kwa kufanya uwekezaji nchini Tanzania ikiwemo Kampuni ya Simu ya Halotel ambayo amesema imechangia kwa kiasi kikubwa huduma za mawasiliano ya simu hasa maeneo ya vijijini.

Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, John Mongella akimkabidi zaiwadi ya kinyago cha alama ya Umoja, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam Phan Dinh Trac, baada ya mazungumzo yao, yaliyofanyika leo, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam
Phan Dinh Trac akiwasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba Jijini Dar es Salaam, leo.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CPV
Phan Dinh Trac akiwasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Jijini Dar es Salaam, leo.
Mkuu wa Utawala Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba Jijini dar es Salaam, Salehe Mhando akimpokea
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CPV Phan Dinh Trac.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, John Mangella akizungumza na mgeni wake
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CPV Phan Dinh Trac alipowasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Jijini Dar es Salaam, leo. Kushoto ni Balozi wa nchi hiyo hapa nchini Vu Thanh Huyen.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya CCM ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Jokate Mwengelo akiwa kwenye mazungumzo hayo. Wapili ni Katibu Msaidizi Mkuu Idara ya Siasa na Mambo ya Nje (SUKI) Jacqueline Lina na Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje Catherine Maleko.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara John Mongella na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CPV
Phan Dinh Trac wakiwa katika mazungumzo jumuishi. Kushoto ni Balozi wa Vietnam hapa nchni Vu Thanh Huyen.
Mazungumzo yakiendelea.
Katibu Jokate Mwengelo akijitambulisha kwenye mazungumzo hayo.
Jacqueline Liana akijitambulisha kwenye mazungumzo hayo.
Mkuu wa Idara ya Usalama na Maadili Makao Makuu ya CCM Sindibad Mwagha, akijitambulisha kwenye mazungumzo hayo.
Salehe Mhando akitambulisha kwenye mazungumzo hayo.
Katibu Msaidizi Idara ya SUKI Viatory Mnyaga akijitambulisha kwenye mazungumzo hayo.
Balozi Vu Thanh Huyen akijitambulisha kwenye mazungmzo hayo.
Mazungumzo yakiendelea.
Washiriki kutoka CCM na Vietnam wakiwa kwenye mazungumzo hayo.
Mazungumzo yakiendelea.
Mwenyekiti wa Kampuni ya Viettel Group ya Vietnam inayomiliki kampuni ya Halotel, akisalimia baada kutambulishwa kwenye mazungumzo hayo.
Katibu Msaidizi Mkuu Idara ya SUKI Jacqueline Liana akitoa maelezo kuhusu zawadi ya kinyago ambacho Trac alikabidhiwa na Mongella.
Mongella akikabidhi kinyago hicho kwa Trac baada ya mazungumzo yao.
Mongella akimkabidhi pia Trac picha ya utalii yenye tembo.
Trac naye akimkabidhi Mongella zawadi ya picha ya ua la Taifa la Vietnam
Mongella akimkabidhi zawadi Balozi Huyen
Kisha Balozi Trac na Mongella wakapongezana kwa zawadi.
Mongella na Trac wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa pande zao, ndani ya ukumbi.
Mongella na Trac wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa pande zao, nje ya ukumbi.
Mongella akiagana na mgeni wake Trac baada ya mazungumzo yao.
Mongella na Jokate wakimpungia Trac wakati akiondoka Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.
 

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages