Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi akiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kigoma Tayri kuanza ziara ya siku mbili katika mkoa huo.
Amelakiwa na viongozi mbalimbali wa chama na serikali wa mkoa huo huku vikundi mbalimbali vikitoa burudani.
'.....................................
Balozi DK Emmanuel Nchimbi anaanza leo ziara ya mikoa mitano ya Kigoma, Geita, Kagera, Mara na Mwanza
Ameanzia leo Mkoa wa Kigoma ambapo pamoja na mambo mengine leo jioni atahutubia mkutano mkubwa wa hadhara mjini Kigoma.
Baada ya kumaliza ziara ya siku mbili katika Mkoa huo ataendelea katika mikoa mingine minne ambayo ni Geita, Kagera, Mara na Mwanza.
Lengo la ziara hiyo ni; Kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020, kuhuisha uhai wa chama, kusikiliza na kutatua kero za wananchi pamoja na kuhamasisha wananchi kujitokeza kuhakiki Taarifa zao na kujiandikisha katika kitabu Cha kudumu Cha Wapiga kura, kwa ajili ya maandalizi ya Uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba mwaka huu.
Katika ziara hii Dk Nchimbi ameambatana na Katibu wa NEC-Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndg. Amos Makalla, Katibu wa NEC-Organaizesheni Ndg. Issa Ussi Haji (Gavu) pamoja na Katibu wa NEC- Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg. Rabia Abdallah Hamid.
Hivi karibuni amemaliza ziara ya siku nne yenye mafanikio makubwa katika mikoa ya Mtwara na Lindi.
Dk Nchimbi akizungumza na wananchi waliofika kumlaki.
Katibu wa NEC-Organaizesheni Ndg. Issa Ussi Haji (Gavu) akijitambulisha kwa wananchi.Dk Nchimbi akizungumza na Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla.
Akizungumza na Katibu wa Oganaizesheni, Issa Ussi Haji Gavu.
Akisalimiana na baadhi ya viongozi waliofika kumlaki
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
MHARIRI
BLOG YA TAIFA YA CCM
0754264203












No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇