LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 4, 2024

CCM YAZIDI KUUSAMBARATISHA UPINZANI, YAVUNA 200 KIGOMA

 

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi, Dk. Emmanuel Nchimbi akipokea kadi za wanachama wa vyama vya upinzani walioamua kujiunga na CCM wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Community Centre Kigoma Mjini Agosti 4, 2024. 

Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Amos Makalla ametangaza kwenye mkutano huo kuwa hadi sasa CCM imevuna  5000 kutoka vya vyama vya upinzani katika mikoa 13 waliyofanya ziara, ambapo katika Mkoa wa Kigoma ambao ni wa 14 wamepokea wapinzani 200 miongoni mwao akiwemo aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu kupita Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutoka mkoa huo, Saprina Sungura na Diwani Patrick Wilizi wa Chama Cha Democratic (DP).

                                      .................

Dk Nchimbi ameanza leo  ziara ya siku mbili katika mkoa huo wa Kigoma ataendelea katika mikoa mingine minne ambayo ni Geita, Kagera, Mara na Mwanza.


Lengo la ziara hiyo ni; Kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020, kuhuisha uhai wa chama, kusikiliza na kutatua kero za wananchi pamoja na kuhamasisha wananchi kujitokeza kuhakiki Taarifa zao na kujiandikisha katika kitabu Cha kudumu Cha Wapiga kura, kwa ajili ya maandalizi ya Uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba mwaka huu.


Katika ziara hiyo Dk. Nchimbi ameambatana na Katibu wa NEC-Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndg. Amos Makalla, Katibu wa NEC-Organaizesheni Ndg. Issa Ussi Haji (Gavu) pamoja na Katibu wa NEC- Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg. Rabia Abdallah Hamid.

Hivi karibuni amemaliza ziara ya siku nne yenye mafanikio makubwa katika mikoa ya Mtwara na Lindi.


Akionesha kadi hizo kutoka upinzani.
Akimpokea Diwani Patrick Wilizi
Saprina Sungura akitaja moja ya sababu zilizomfanya ajiunge na CCM kuwa ni kupendezewa na utendaji wa Rais Samia Suluhu Hassan wa kuwaletea maendeleo watanzania ikiwemo Mkoa wa Kigoma.
 

Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Amos Makalla akiwatangaza wapinzani waliojiunga na CCM.

Katibu wa Oganaizesheni, Issa Ussi Haji (Gavu) akiwapongeza wananchi wa Mkoa wa Kigoma kujitokeza kwa wingi kuhakiki na kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika zoezi lililofanyika mkoani humo hivi karibuni. Amewataka wote waliojiandikisha kujitokeza kwa wingi katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba, 2024.

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages