Mbunge wa Njombe Mjini, Deodatus Mwanyika ameitaka serikali kufanya haraka kuweka umeme katika baadhi ya mitaa ya jimbo hilo ikiwemo ya Unguja na Pemba.
Aidha ameitahadharisha Wizara ya Nishati kuhusu ujenzi wa viwanda vingi vya nguzo za saruji kwa kutowakumbuka wananchi waliowekeza kwa kupanda miti mingi ya nguzo hali ambayo itawasababishia umasikini.
Pamoja na mambo mengine ametoa ombi hilo alipokuwa akitoa mchango wakati wa kujadili Bajeti ya Wizara ya Nishati bungeni Dodoma Aprili 25, 2024.
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
MHARIRI
BLOG YA TAIFA YA CCM
0754264203
No comments:
Post a Comment
ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇