Na Dismas Lyassa, Kibaha
MBUNGE wa Jimbo la Mjini, Silvestry Koka ameahidi kulivalia njuga suala la huduma ya nishati ya umeme na maji ambalo limekuwa kero katika baadhi ya maeneo ya jimbo hilo.
Akizungumza kwenye semina ya mafunzo kwa wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Kibaha Mjini amesema lengo kubwa ni Kuhakikisha anawatatulia wananchi changamoto zinazowakabili katika sekta mbali mbali.
Kadhalika aliwaomba wananchi waweze kuendelea kushirikiana na Serikali ili waweze kupatiwa miradi mbali mbali ya kimaendeleo kwa manufaa ya wananchi wa Jimbo la Kibaha mji na Taifa kwa ujumla.
Mbunge huyo hakusita kuwakumbusha viongozi kijitahidi kwa hali na mali katika kuongeza idadi ya wanachama lengo ikiwa ni katika kukiimarisha chama zaidi kiweze kushinda katika chaguzi mbali mbali.
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇