Na Dismas Lyassa
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (Zanzibar), Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK. Hussein Ali Mwinyi amewaasa wanachama wa
chama hicho kuimarisha mshikamo na kuachana na makundi.
Dk Mwinyi alisema kunapokuwa na chaguzi kama ule wa ndani ya chama uliokwisha
mwaka jana, ni kawaida wagombea kuwa na makundi; huyu atamtaka yule na mwingine
atamtaka huyu, lakini mara baada ya chaguzi kumalizika, makundi yote ni lazima
yavunjwe ili kushirikiana kwa pamoja kuimarisha chama.
Kiongozi huyo ameonyesha kukerwa na wenye kuendekeza makundi, akaagiza wale
wanaobainika kuendelea kukiuka taratibu na kuchangia kuwepo kwa makundi kuitwa
na kuchukuliwa hatua na Kamati za maadili ili kuhakikisha nidhamu na mshikamano
ndani ya chama unatamalaki.
Dk. Mwinyi ameyasema hayo katika ziara yake Mkoa wa Mjini Magharibi, yenye lengo
la kukiimarisha chama na kutembelea miradi mbalimbali kukagua utekelezaji wa
Ilani ya Chama akiambatana na viongozi mbalimbali wa Serikali na chama akiwamo Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho (Zanzibar) Mohammed Said Mohammed (Dimwa).
Your Ad Spot
May 7, 2023
Home
Unlabelled
DK MWINYI AFANYA ZIARA, AWAASA WANACCM KUIMARISHA MSHIKAMANO
DK MWINYI AFANYA ZIARA, AWAASA WANACCM KUIMARISHA MSHIKAMANO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇