Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akisalimiana ns Rais wa Burundi wasili Rais wa Burundi Mheshimiwa Evariste Nayishimiye, baada kuwasili Ikulu ya nchi huyo mjini Bujumbura, leo Mei 6, 2023.
Makamu wa Rais amewasili nchini humo leo kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 11 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Mpango wa Amani, Usalama na Ushirikiano kwa ajili ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Ukanda wa Maziwa Makuu unaofanyika Bujumbura nchini Burundi.
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇