Zanzibar, leo
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK. Hussein Ali Mwinyi amesema baada ya uchaguzi kumalizika ni muhimu kwa Chama na Wanachama kujenga umoja, kwa kuondoa makundi yote na kushirikiana kwa pamoja.
Amesema, wale ambao wanaendelea kukiuka taratibu na kuchangia kuwepo kwa makundi wanapaswa kuitwa na kuchukuliwa hatua na Kamati za maadili ili kuhakikisha nidhamu na mshikamano ndani ya chama unatamalaki.
Dk. Mwinyi ameyasema hayo katika mkutano wa viongozi wa CCM ngazi ya Shina , Majimbo, Wilaya na Mkoa uliofanyika katika ukumbi wa Picadilly, Kombeni, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini Magharibi, mwanzono mwa ziara yake leo ya kukiimarisha chama na kutembelea miradi mbalimbali kukaguautekelezaji wa Ilani ya Chama.
Ziara hiyo ya kukagua utekekezaji wa Ilani ya CCM kwenye miradi na kukiimarisha Chama ni ya kwanza kwake tangu awe Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar.
Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akisisitiza jambo wakati alipokuwa akizungumza katika Mkutano wa Mabalozi na Halmashauri Kuu za CCM Majimbo ,Wilaya na Mkoa wa Magharibi Kichama katika ukumbi wa Piccadiliy Kombeni Wilaya Magharibi "B"leo.
Washiriki katika ngazi mbali mbali katika Mkutano wa Mabalozi na Halmashauri Kuu za CCM Majimbo,Wilaya na Mkoa wa Magharibi Kichama wakimsikiliza Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi(hayupo pichani) wakati alipokuwa akizungumzanao leo katika ukumbi wa Piccadiliy Kombeni Wilaya Magharibi "B" (Picha na Ikulu, Zanzibar)
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇