LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Apr 12, 2023

MBUNGE SUBIRA MGALU AWAPA CHEREHEANI 35 KINAMAMA KIBITI NA KIBITI WAJIKWAMUE KIUCHUMI

Na Scolastica Msewa, Kibiti

MBUNGE wa viti maalum kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani Mheshimiwa Subira Mgalu amekabidhi Wanawake wa wilaya ya Rufiji na Kibiti vyerehani 35 kwa lengo la kuwainua kiuchumi wana mama hao.

Akizungumza mara baada ya kuwakabidhi vyerehani hivyo Mgalu alisema kuwa Wanawake wengi wamekuwa tegemezi sana kutoka kwa wanaume zao hivyo vyerehani hivi vinakwenda kuwa chachu ya ukuzaji uchumi wa wanawake hao na ndani ya jumuiya ya UWT.

Walionufaika na mgao wa Vyerehani hivyo ni wenyeviti wa kila kata na makatibu wa kila kata wa Jumuiya ya UWT pia ofisi za wilaya zimepata vyerehani vitatu ili nao waweze kusimama kiuchumi kwa kuanzisha miradi ya ushonaji.

"Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan amekuwa akisisitiza juu ya wanawake kuweza kujisimamia katika masuala yetu ya kiuchumi ndio maana nimewapatia mitaji hii ili muweze kukuza uchumi wenu mmoja mmoja au kikundi"Alisema Subira Mgalu.

Aidha amewakumbusha wanawake kuwa mstali wa mbele katika kukemea ukatili wa kijinsia unaoendelea kwa watoto wetu kwani Taifa letu halikuwai kuwa na mambo ya ajabu katika maadili ,hivyo kila mzazi asimamie maadili kwa mtoto wake na watoto wa mwenzie.

Mbunge huyo amewataka wanawake hao kuvitumia vyerehani hivyo ili viweze kuwainua kiuchumi na kuondokana na tegemezi ya waume wao.

Naye Mwajuma Said ambaye ni mkazi wa Rufiji amempongeza Mhe. Subira Mgalu kwa jinsi ambavyo amekuwa mstali wa mbele katika kuwapambania wanawake wa Mkoa wa Pwani.

Aidha amemwakikishia kuwa uchumi wa wanawake unakwenda kupanda kutokana na kupewa mashine hizo na sio lazima wote tuwe washinaji hata kuvikodisha inawezekana.

Kwa Upande Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Kibiti Tatu Mkumba amesema kuwa Mgalu ni kiongozi mwenye maono ya mbali katika jumuiya hiyo.

Aidha amewataka Wanawake wote ndani ya Mkoa wa Pwani kuendea kumuombea kwa Mungu ili aweze kufanikiwa na kuzidi kutuletea neema zaidi.
 

Mbunge Viti maalumu mkoa wa Pwani Subira Mgalu (kulia) akimkabidhi Moja ya vyerehani 35 Mwenyekiti wa UWT Kibiti Tatu Mkumba kwaniaba ya Wanawake wa UWT Wilaya ya Kibiti na Rufiji katika hafla fupi iliyofanyika wilayani Kibiti mkoani Pwani. (Na Scolastica Msewa).

Mbunge wa Viti maalumu mkoa wa Pwani Subira Mgalu (wa nne kuanzia kulia) katika picha ya pamoja wakati wakiimba Wimbo wa CCM na Wanawake wa UWT Kibiti baada ya kukabidhi vyerehani 35 KWA Wanawake wa Wilaya ya Kibiti na Rufiji katika hafla iliyofanyika wilayani Kibiti mkoani Pwani (na Scolastica Msewa)
 

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages