LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 2, 2023

KATIBU MKUU WA CCM AWAPONGZA VIONGOZI WA CHAMA IRAMBA - SINGIDA

 VIONGOZI IRAMBA WAONGEZA WANACHAMA

Na HEMEDI MUNGA

KATIBU mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo amempongeza Mwenyekiti wa shina namba sita katika kata ya Ulemo, Evangelina Samweli kwa kuongoza wanachama wa chama hicho na kazi kubwa ya kujenga chama wanayoendelea nayo katika wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Chongolo amesema Mwenyekiti huyo na katibu wake wanaongoza vizuri kwa kuongeza wanachama 38 kwa kipindi kifupi na kazi inaendelea.

Katibu Mkuu huyo, alitoa pongezi hizo leo wakati alipofanya ziara ya kujenga uhai wa chama katika wilaya ya Iramba mkoani humo.

Halikadhalika, Chongolo alimuagiza mkuu wa wilaya hiyo, Suleiman Mwenda kujibu baadhi ya kero zilizoibuka katika ziara hiyo.

Akijibu kero zilizoibuka katika ziara hiyo mbele ya katibu mkuu huyo, Mkuu wa wilaya hiyo, Suleiman Mwenda aliwatoa hofu watu wenyemahitaji maalumu kuwa serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ilikwishatoa maagizo ya kujaliwa.

Mwenda alisema Halmashauri hiyo iliishatenga takribani sh 4.3 milioni kwa lengo la kuhakikisha kundi hilo linakaa vikao vyao kwa sababu ya kupanga mipango yao kwa mustakabali wa maisha yao.

Aidha, alifafanua kuwa serikali sikivu ya Dk. Samia ilishatoa maelekezo, hivyo wanayafanyia kazi kwa umakini mkubwa.

‘’Ni lengo la serikali kuona watu wote wanapata haki na huduma sawa, hivyo tunahakikisha kundi hili muhimu linapata mahijati kulingana na utaratibu uliowekwa katika ilani ya Chama Cha Mapinduzi,’’ alisema.

Aidha, aliongeza katika asilimia 10 za mikopo itolewayo na serikali kundi hili la walemavu ni miongoni mwa wanufaika wa mkopo huo.

 ‘’Ninashukuru Mhe, Katibu Mkuu ninaomba nikuhakikishie kuwa walemavu tunawapa mikopo ya asilimia mbili toka kwenye asilimia 10, na tayari vipo vikundi vya walemavu vimepatiwa mikopo,’’alisema.

Pia, alisema kuhusu vikao wanavyotakiwa kukaa walemavu Halmashauri imekwisha tenga takribani sh 4.3 milioni kwa mwaka wa fedha 2022/2023, hivyo watakaa vikao vyao

Akizungumzia kuhusu chakula kwa lengo la kuhakikisha ufaulu unaongezeka kwa shule zote, alisema wameweka utaraibu wa kuhakisha chakula cha wanafunzi kinapatikana.

‘’Ni makubaliano ya vikao kuhakikisha watoto katika shule za msingi na sekondari wanapata chakula kutokana na michango yetu,’’ alisema.

Hatua hiyo inatokana na utafiti walioufanya na kugundua kuwa uwepo wa chakula shuleni unasabisha watoto kuelewa na hatimaye wanafaulu katika masomo yao.


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo akipata maelezo toka kwa Doktari Timothy  Sumbe kulia, kushoto kwa katibu mkuu ni Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba na mwisho kushoto ni mkuu wa wilaya hiyo, Suleiman Mwenda. (Picha na ofisi ya mkuu wa wilaya)

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda akiwa katika mkutano pindi Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo alipotemelea wilaya hiyo leo. (Picha na ofisi ya mkuu wa wilaya)

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda akiteta jambo na mmoja wa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika mkutano pindi Katibu Mkuu wa Chama hicho, Daniel Chongolo alipotemelea wilaya hiyo leo. (Picha na ofisi ya mkuu wa wilaya)




No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages