Ikulu, Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Zanzibar ina mengi ya kujifunza uzoefu na weledi kutoka nchi ya Ufilipino hasa kwenye sekta za mafuta na gasi, afya, utalii na uvuvi .
Pia Dk.Mwinyi amemuomba Balozi wa Ufilipino kuitangaza Zanzibar katika fursa mbalimbali ambazo zinapatikana visiwa humo.
Dk. Mwinyi aliyasema hayo leo tarehe 02 Machi, 2023 Ikulu Zanzibar alipokutana na Balozi wa Ufilipino Tanzania ,Marie Charlotte G.Tang aliyefika kujitambulisha.
Naye, Balozi Marie Charlotte G.Tang amesema ataongeza uhusiano kati ya Ufilipino na Tanzania pia amekubali kuitangaza na kuwashawishi wawekezaji kutoka nchini mwake kuja Zanzibar kuangalia fursa za Uwekezaji zinazopatikana kutokana na kufanana mazingira kati ya Ufilipino na Zanzibar .Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar Mhe Dk. Hussein
Ali Mwinyi (kulia) alipokuwa katika mazungumzo na Balozi wa Ufilipino
Nchini Tanzania Mhe.Marie Charlotte G.Tang,wakati alipofika Ikulu
Jijini Zanzibar leo kujitambulisha.
Your Ad Spot
Mar 2, 2023
RAIS DK. MWINYI: ZANZIBARA INA MENGI YA KUJIFUNZA UZOEFU KUTOKA UFILIPINO
Tags
featured#
Zanzibar#
Share This
About CCM Blog
Zanzibar
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇