Mtafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Macklina
Komba akimfanyia usajili mwananchi wa Mkoa wa Geita aliyefika katika Hospitali
ya Rufaa ya Kanda Chato (CZRH) kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na matibabu ya
moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano inayoendelea katika Hospitali hiyo. Wataalam wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na
wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato (CZRH) wakiwafanyia vipimo vya
awali wananchi waliofika katika Hospitali hiyo kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi
na matibabu ya moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano inayoendelea katika
Hospitali hiyo. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Janeth Mmari
akimwelezea namna ya kujikinga na magonjwa ya moyo mkazi wa Chato aliyefika
katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na
matibabu ya moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano inayoendelea katika
Hospitali hiyo. Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kulwa
Richard akimpima wingi wa sukari mwilini mkazi wa Chato aliyefika katika
Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na matibabu
ya moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano inayoendelea katika Hospitali hiyo. Afisa Muuguzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato (CZRH)
John Daniel akimpima Shinikizo la damu mkazi wa Chato aliyefika katika
Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na matibabu
ya moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano inayoendelea katika Hospitali hiyo.
Baadhi ya wananchi wa Mkoa wa Geita wakiwa katika foleni ya
kupatiwa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo wakati wa kambi maalum ya siku
tano inayofanywa na wataalam wa afya kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato (CZRH). Picha na: JKCI
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇