Na Mwandishi Maalum, Dodoma.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) Jaji Dk. Eliezer Feleshi, ameishukuru Serikali kwa uamuzi wake wa kuijumuisha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na Wizara nyingine ambazo zimepewa fedha za kujenga Majengo ya kudumu katika Mji wa Serikali wa Mtumba, Jijini Dodoma.
Ametoa shukrani hizo leo, Alhamisi, Julai 14, 2022, alipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo jipya la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika mji huo wa Serikali.
“Ninawashukuru sana Rais wa Awamu ya Sita Samia Suluhu Hassan na Mtangulizi wake Hayati Dk. John Magufuli kwa maono yao na utambuzi wao wa kuiunganisha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wizara mbalimbali katika awamu ya kwanza na ya pili ya ujenzi wa majengo ya kudumu hapa Mtumba.Hii ni heshima kubwa kwetu na hasa kwa kuzingatia unyeti wa majukumu yetu”, akaeleza Mhe. AG
Katika ziara yake hiyo ambayo alikuwa ameambatana na Menejimenti yake, AG Feleshi amesema uamuzi wa Serikali wa kuwa na majengo ya kudumu ya serikali katika Mji wa Serikali wa Mtumba ni uamuzi wa kihistoria kwa vizazi na vizazi na umeufanya mji huo wa Serikali kuwa kivutio cha kitalii.
“ Majengo haya ni ya kudumu, ni historia kwa vizazi na vizani na kwa miaka mingi ijayo. Kwa hiyo nanyi Wakandarasi ambao mmepata fursa ya kujenga majengo haya lazima mjivunie historia hii kwa kufanya kazi wa uadilifu na kwa wakati, kwa sababu mnaandika historia”, akasisitiza AG Feleshi.
Jengo la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali lenye ghorofa tano na umbo la herufi 'Y' linajengwa na Mkandarasi SUMA JKT Kanda ya Kati na licha ya kuwa na umbo la herufi Y, litakapokamilika litakuwa ni kati ya majengo ya kipekee na makubwa matatu katika majengo yote ya serikali yanayojengwa katika mji huo wa serikali.
AG Feleshi pamoja na kuridhishwa na namna kazi ya jenzi wa mradi huo , memtaka Mkandarasi kutosita kumpatia taarifa endapo kutakuwa na uchelewesashi wowote au urasimu kutoka pande zote mbili ( mteja na mkandarasi) ili aweze kuchukua hatua zozote.
“Mmenieleza hapa kwamba kwa sasa hamna changamoto kubwa, ila niwaombe kama kutakuwa na changamoto yoyote iwe kutoka Ofisini kwangu au kutoka Jeshini msisite kunijulisha ili hatua za mapema zichukuliwe. Lakini sisi ni wasimamizi wa Sheria, pia nisingependa kuona kunajitokeza matatizo yoyote ya kisheria kwenye mradi huu”, akasema AG Feleshi.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali pia alijiridhisha kwamba fedha za utekelezaji wa mradi huo zimekuwa zikitolewa kwa wakati kila Mkandarasi anapowasilisha hati zake ( Certificate) na kwamba hakuna malimbilizo yoyote.
Awali akitoka maelezo ya maendeleo ya mradi huo Mshauri Mwelekezi Mhandisi William Sele kutoka Wakala wa Majengo ( TBA) alimweleza Mhe. AG na Ujumbe wake kwamba kazi ya ujenzi wa jengo hilo unakwenda vizuri kwa asilimia 26 ya ujenzi na kwamba hawategemei kupata changamoto kubwa labda uhaba wa mali ghafi hapo baadaye.
Mhandisi Sele pia amesema sasa hivi TBA inajitahidi sana katika usimamizi wa kazi zake ili kwenda na wakati na kuondoa malalamiko ya kwamba TBA wamekuwa wakishelewesha utekelezaji na ukamilishaji wa miradi mbalimbali.
“Sasa hivi kwa kweli tumejipanga vizuri, kazi zinakwenda kwa wakati, vibali vinatolewa kwa wakati, huko nyuma TBA tulikuwa tunalalamikiwa kwa ucheleweshaji wa vibali na mengineyo kama hayo, sasa tupo vizuri”, akasema Mhandisi Sele
Your Ad Spot
Jul 14, 2022
Home
featured
Kitaifa
AG FELESHI AKAGUA UJENZI WA JENGO LA OFISI YA AG KATIKA MJI WA MTUMBA, AWASHUKURU RAIS SAMIA, JPM KWA MAONO
AG FELESHI AKAGUA UJENZI WA JENGO LA OFISI YA AG KATIKA MJI WA MTUMBA, AWASHUKURU RAIS SAMIA, JPM KWA MAONO
Tags
featured#
Kitaifa#
Share This
About Bashir Nkoromo
Kitaifa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇