CCM HQ, Dodoma
Chama Cha Mapinduzi Kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mbunge wa zamani wa Chama Cha Wananchi (CUF) na Mkurugenzi wa Fedha na Mipango Khadija Makontena kilichotokea leo Alhamisi 14 Julai, 2022.
Taarifa iliyotolewa Katibu Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka imesema kufuatia kifo hicho, Mwenyekiti wa CCM Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Samia Suluhu Hassan amemtumia salaam za pole Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF ) Profesa Ibrahim Lipumba, familia, ndugu na jamaa.
“Bi Khadija tokea kuanzishwa mfumo wa Vyama Vingi vya siasa amekuwa akishiriki kikamilifu katika uwanja wa siasa za ndani na nje ya chama chake huku akiamini siasa za umoja na maelewano.
Mwenyezi Mungu awape ustahamilivu na subira katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
Sisi Sote niwa Mwenyezi Mungu na kwake tutarejea", amesema Mwenyekiti wa CCM Rais Samia.
Mwenyekiti wa CCM Rais Samia |
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇