LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jun 23, 2022

MAJALIWA ZIARANI ARUSHA NA TANGA KUONA AWAMU YA PILI WA WANAOHAMA KUTOKA HIFADHI YA NGORONGORO

Na Mwandishi Maalum

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Juni 23, 2022 anafanya ziara ya siku moja katika mkoa wa Arusha na Tanga ambapo atashuhudia zoezi la awamu ya Pili ya wananchi takribani 117 kutoka kaya 27 wanaohama kwa hiari yao wenyewe kutoka katika eneo la hifadhi ya Ngorongoro kuelekea kijiji cha Msomera, Handeni 


Mheshimiwa Majaliwa pia atakagua Makazi na miundombinu ya huduma kwa wananchi katika kijiji cha Msomera, Handeni mkoani Tanga


Pia Mheshimiwa Majaliwa atakagua alama zilizowekwa kubainisha eneo la hifadhi ya pori tengefu la Loliondo la Kilometa za mraba 1500.


Mheshimiwa Majaliwa amewapongeza wakazi hao kwa maamuzi yao ya kuhamia Katika kijiji cha Msomera ambapo amewahakikishia kwamba Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan ipo pamoja nao.



No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages