LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 25, 2021

WAZIRI NDAKI: NI AJABU MTANZANIA HUNYWA KIJIKO KIMOJA BADALA YA LITA 200 ZA MAZIWA KWA MWAKA+video

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Dkt Mashimba Ndaki leo Novemba 25, 2021, amezungumza katika mkutano na vyombo vya habari jijini Dodoma, kuelezea tulikotoka, tulipo na tunakoelekea zikiwemo changamoto na mafanikio ya sekta hiyo  kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara.


Pamoja na kuelezea mambo mbalimbali kuhusu hatua ilizopiga sekta hiyo, amesema kuwa kwa kawaida kila Mtanzania anatakiwa kila mwaka kula nyama zaidi ya kilo 50 lakini anakula kilo 15 tu, na kwa upande wa maziwa anatakiwa kunywa zaidi ya lita 200, lakini anakunywa wastani wa kijiko kimoja....

Waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo ambapo baadhi hupata kuuliza maswali.





Waziri Ndaki akijadiliana jambo na Afisa Habari wa Idara ya Habari-MAELEZO, Immaculate  Makilika baada ya kumalizika kwa mkutano huo ulioongozwa na afisa huyo.
Waziri Ndaki akiwa na viongozi wengine wa wizara hiyo.

 Waziri Ndaki akiondoka kwa furaha baada ya kumalizika kwa mkutano huo.


PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA


Mdau, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video, Waziri Ndaki akielezea umuhimu wa watanzania kuongeza kiwango cha kula nyama na unywaji maziwa kwa mwaka...

Imeandaliwa na Richard Mwaikenda 
Mhariri Blog ya Taifa ya CCM 
0754264203

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages