LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 15, 2021

WAKAZI JIJINI DODOMA WAHIMIZWA KULIMA KILIMO CHENYE TIJA


WAKAZI jijini hapa wametakiwa  kujikita katika kilimo chenye tija kwani Tanzania imejaaliwa ardhi ya kutosha, na kuachana na ile dhana ya kwamba kilimo kinawafaa watu wasio na ajira pekee.

Hayo yamesemwa  na Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mwanahamisi Munkunda kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa  wa Dodoma Antony Mtaka wakati akifungua maonesho ya siku saba  ya kilimo kanda ya kati  yanayoendeshwa na Kampuni ya  Jenga Afya Tokomeza Umasikini (JATU PLC) yajulikanayo kama wiki ya mavuno.

Amesema Jamii hasa vijana wanadhani ya kwamba kilimo ni cha watu wasio na shughuli zingine za kufanya  kitu ambacho si sahihi kwani wanaweza wakalima huku wakiwa  ofisini au vyuoni wakiendelea na majukumu yao wakalima  na kampuni  ya  JATU.

“Sisi kama Taifa Tumekuwa  na uhaba wa mafuta kipindi kilichopita tukaja na mikakati ya kulima zao la alizeti kwenye mikoa  mitatu ya Singida Dodoma  na Simiyu kwa kuanza  kuzalisha mbegu tani laki 5 kwaajili ya kuondokana na uhaba wa mafuta wakati  huu ndio ulikuwa mzuri kuchangamkia fursa hizi”.amesema Mwanahamis

Na kuongeza kusema kuwa “Sasa kumbe tulikuwa tunawaza sawa sawa  kama JATU mnavyowaza ifike mahala sasa tuwe na dhana ya nilime nijilishe na siyo tusubiri watu wengine walime na hutujui wanalima  kwa aina gani mbegu gani wanatumia” amesema Mwanahamis

Kwa upande wake Meneja  kutoka Taasisi ya JATU Mohamed Simbano amesema kampuni hiyo ilianzishwa na vijana wa kitanzania ambao ni wahitimu wa chuo kikuu cha Dar es salaam lengo likiwa ni kuhakikisha ustawi wa maisha ya watu kiafya kutokana na bidhaa bora na asilia zinazotokana na kampuni hiyo.

“Pia inatoa suluhisho katika kupunguza umasikini kwa kutumia ipasavyo  rasilimali watu kilimo cha kisasa na  shughuli za viwanda pamoja na kugawana faida na mlaji wa mwisho”amesema Simbano.

Akizungumzia kuhusu maonesho hayo amesema lengo la maonesho hayo ni kuweza kuhakikisha  jamii kila  mkoa wilaya hasa wakulima ambao wengi wapo katika  mikoa mbalimbali na wengi wamekuwa wakiomba  kampuni hiyo iweze kuwafikia.

“Lengo letu ni  ili maeneo yote  ili kujifunza namna ya kuimarisha na kuchochea ukuaji ukuwaji wa sekta ya kilimo kama ilivyo sera ya kilimo na mikakati ya serikali katika kuhimiza taasisi kuweka nguvu katika kilimo kwa kuwa ndo sekta inayochangia mkwa sehemu kubwa pato la taifa”

Hata hivyo maonesho  hayo ya  kilimo kanda ya kati yanatarajia kufungwa tarehe 20 october huku yakiwa yamebebwa na kauli mbiu isemayo wiki ya mavuno  anza na ekari moja

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages