LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 28, 2021

HOTELI MPYA YA KISASA YA MBUNGE SANGA YAZIDI KULIPAMBA JIJI LA DODOMA+video

Hoteli mpya ya kisasa ya DS inazomilikiwa na Mbunge wa Makambako, Deo Sanga ikiwekwa maji ya baraka (Wakfu) eneo la Kilimani, Tambukaleli jijini Dodoma.  Tukio hilo lililofuatiwa na uwekaji wa jiwe la msingi ni sehemu ya maandalizii ya ufunguzi unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

Mbaadhi ya majengo ya hoteli hiyo ambayo  licha ya kulipendezesha Jiji la Dodoma ambalo ndiyo Makao Makuu ya Nchi, itasaidia kuongeza ajira na kuinua uchumi wa mkoa huo na Taifa kwa ujumla.
Viongozi wa Dini wakiazaombea maji ya baraka tayari kuweka wakfu kwenye hoteli hiyo.


Maji ya baraka yakinyunyiziwa kwenye majengo mbalimbali ya hoteli hiyo.


Baadhi ya wageni waalikwa kutoka sehemu mbalimbali wakiwa katika  ibada maalumu ya  uwekaji wa wakfu.

Kwaya ikitumbuiza wakati wa ibada maalumu ya uwekaji wakfu hotelini hapo.
Mshereheshaji maarufu MC Peter Mavunde akionesha umahiri wa kupiga kinanda wakati kwaya hiyo ikitumbuiza.
Baadhi ya wageni waalikwa


Mmiliki wa hoteli hiyo, Deo Sanga (kulia), akibadilishana mawazo na wageni waalikwa.

Wakurugenzi wasaidizi wa Hoteli hiyo, Agustino Msigwa (kushoto) na Ami Ilomo wakijadiliana jambo wakati wa ibada hiyo ili kuweka mambo sawa.

Deo Sanga akijadiliana jambo na wageni waalikwa.
PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA

Mdau, nakuomba uendelee kusikiliya/kuona kupitia kwenye clip hii hapa chini ujue yaliyojiri wakati wa ibada hiyo......

 

IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
 MHARIRI BLOG YA TAIFA YA CCM 
0754264203

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages