LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jun 25, 2021

SELEMANI MWENDA AAPISHWA KUWA MKUU WA WILYA YA IRAMBA, AAHIDI KUTIMIZA MATARAJIO YA RAIS SAMIA, AMSHUKURU KUMTEUA.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Binilith Mahenge akimuapisha Mkuu Mpya wa Wilaya ya Iramba Selemani Mwenda mjini Singida, leo. Mwenda aliteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan juzi, kuchua nafasi ya Kenan Kihongosi aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).
 
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Binilith Mahenge akimkabidhi Ilani ya CCM Mkuu Mpya wa Wilaya ya Iramba Selemani Mwenda mjini Singida,baada ya kumuapish leo. 

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Binilith Mahenge akizungumza baada ya kumuapisha mkuu huyo wa wilaya.

Mkuu Mpya wa Wilaya ya Iramba Semani Mwenda akizungumza baada ya kuapishwa.

Baadhi ya viongozi wa Dini Wilani Iramba wakiwa kwenye hafla hiyo ya Uapisho. .

Wanandugu wa Mkuu huyo wa Wilaya ya Iramba wakiwanye hafla hiyo

Baadhi ya Viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Iramba wakiwa kwenye hafla hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk.Binilith Mahenge, (katikati) akiwa katika picha ya kumbukumbu na Wakuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskas Muragili (kushoto) Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Jerry Muro  (kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Iramba Selemani Mwenda  (wa pili kushoto), baada ya kumuapisha (Mwenda) na wa pili kulia ni Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dorothy Mwaluko.

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Selemani Mwenda akiwa na Wanafamilia yake baada ya kuapishwa


Iramba, jana

MKUU wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge amesema ishara ya utawala uliotukuka ni amani na utulivu katika maeneo ya kazi na si vinginevyo.


Dkt. Mahenge ameyasema hayo  baada ya kumuapisha Mkuu Mpya wa Wilaya ya Iramba Selemani Mwenda ambaye ameteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuongoza wilaya hiyo.


“Jambo la msingi ninalopenda kukuambia hakikisha kuna amani na utulivu katika wilaya yako hata ukifanya makubwa mazuri kiasi gani kama hakuna amani na utulivu mambo hayo yatafunikwa na makosa,” alisema Mahenge.


Alisema ni wajibu wa viongozi kuhakikisha ulinzi, usalama na amani vinatamalaki muda wote kuzunguka maeneo yao.


Aliongeza kwamba kazi ya kiongozi wa umma, pamoja na mambo mengine ni kuhamasisha maendeleo katika kila nyanja.


“Niwaombe sana vijana wangu wakati mnatekeleza majukumu yenu zingatieni akili za kuambiwa changanya na za kwako,” alisema Dkt. Mahenge.


Mahenge aliahidi kuwapa ushirikiano wakuu wote wa wilaya mkoani hapa lakini kwa wale watakao kuwa wachapa kazi na kuwa afadhari watofautiana kwenye misingi ya utekelezaji wa kazi watakaa na kuamua kipi wakifanye na si majungu.


Akizungumza baada ya kuapishwa Selemani Mwenda alitoa shukurani kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini kushika nafasi hiyo na kuahidi kukidhi matarajio ya nafasi hiyo kwa kwenda kuwatumikia wananchi wa Iramba na kufuata kiapo alichoapa cha utumishi.


Mkuu wa wilaya ya Singida, Mhandisi Paskas Muragili na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Jerry Muro wakizungumza kwa nyakati tofauti katika hafla ya kumpokea Mwenda waliahidi kumpa ushirikiano wakati wa kutekeleza majukumu yake ya kuwaletea wananchi wa Wilaya ya Iramba maendeleo.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages