LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 4, 2021

RC MAHENGE AWAPIGA MARUFUKU WAATHIRIKA WA MAFURIKO NKUHUNGU KUREJEA KWENYE MAKAZI YAO

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk. Binilith Mahenge akitoa agizo  watu wote waliohama kwenye nyumba zao zilizoathirwa na mafuriko eneo la Nkuhungu, kutorejea tena katika nyumba hizo kwa usalama  wa maisha yao hata kama maji yatakauka.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA
Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru akijadiliana jambo na baadhi ya viongozi wa waathirika wa mafuriko eneo la Nkuhungu, jijini Dodoma .
RC Mahenge akizungumza na wananchi wa eneo hilo alipokwenda kuwatembelea
Baadhi ya nyumba ambazo watu wamezihama baada ya kukumbwa na mafuriko.




Wakazi wa eneo hilo  wakitega samaki kwa ajili ya kitoweo


Na Richard Mwaikenda, Dodoma

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk. Binilith Mahenge amewataka watu wote waliohama kwenye nyumba zao zilizoathirwa na mafuriko eneo la Nkuhungu, kutorejea tena katika nyumba hizo kwa usalama  wa maisha yao hata kama maji yatakauka.


Dk. Mahenge ametoa agizo hilo alipotembelea kuona athari za mafuriko katika eneo hilo linalokadiriwa kuwa na kaya 600.


Amewataka waathirika ambao baadhi hadi sasa hawana mahali pa kuishi, kuacha kung'ang'ania kuishi eneo hilo ambalo hivi sasa ni hatarishi kwa maisha yao.


Katika hatua nyingine, Dk. Mahenge ameunda kikosi kazi kitakachofanya tathmini ya kujua nyumba zote zilizopo kwenye maji zikiwemo zilizopewa vibali vya ujenzi na wananchi waliovamia kujenga, ili serikali iangalie  namna ya kuwahamishia maeneo mengine salama.


Ndugu, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia kwenye clip hii ya video ujue kwa kina yaliyozungumzwa na Dk. Mahenge, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma,  Joseph Mafuru, Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde pamoja na waathirika wa eneo hilo....


Imeandaliwa na Richard Mwaikenda 
 Mhariri Blog ya Taifa ya CCM
 0754264203

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages