LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 4, 2021

RAIS DK.MWINYI AWAAPISHA MAWAZIRI ALIOWACHAGUA HIVI KARIBUNI


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Mhe. Nassor Ahmed Mazrui kuwa Waziri wa Afya,Ustawi wa Jamii,Wazee Jinsia na Watoto Zanzibar, hafla hiyo ya kuapishwa imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 4-3-2021.

 



MAWAZIRI Wateuli wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar ( ZRB) wakiwa katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar wakisubiri kuapishwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) hafla hiyo ya kuapishwa imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 4-3-2021.

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akiwa amesimama wakati ukipigwa Wimbo wa Taifa kabla ya kuaza kwa hafla ya kuapishwa kwa Mawaziri na Kamishna wa ZRB katika ukumbi wa Ikulu  walioteuliwa hivi.

VIONGOZI wa Serikali na Mawaziri Wateuli wakiwa wamesimama wakati ukipigwa wimbi wa Taifa na wa Afrika Mashariki kabla ya kuaza kwa hafla ya kuapisha, (kulia) Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman na (kushoto) Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Othman Makungu na Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Mhe. Dkt, Mwinyi Talib Haji.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Dkt. Saada Mkuya Salum kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, hafla hiyo ya kuapishwa imefanyika leo 4-3-2021 katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akimkabidhi hati ya kiapo Waziri wa Afya Ustawi wa Jamii, Wazee,Jinsia na Watoto Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui, baada ya kumaliza kula kiapo, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Mhe. Omar Said Shaaban, kuwa Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages