LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 5, 2021

MARUFUKU KUINGIA KANISANI BILA KUNAWA MIKONO-ASKOFU DK. CHANDE+video

 Na Richard Mwaikenda, Dodoma

ASKOFU wa Kanisa la EAGT Nazaret, Dk. Evance Chande  amepiga marufuku waumini kuingia kanisani,ofisini kwake  bila kunawa mikono ikiwa ni tahadhari dhidi ya janga la corona.


Akihubiri hivi karibuni katika kanisa lake lililopo Ipagala, jijini Dodoma, Askofu Dk. Chande amewatahadharisha waumini wake kuwa pamoja na kumtegemea Mungu katika mapambano dhidi ya janga la corona, wasiache mlango wazi kwa kusahau tahadhari zingine ikiwemo kunawa mikono na kuvaa barakoa walizozishona wenyewe.


Amesema kwa kujali hilo ndiyo maana katika milango ya kuingilia kanisani na ofisini kwake ameweka maji na sabuni ili kabla ya waumini kuingia wanawe mikono.


"Unapomtegemea Mungu, usiache mlango wazi. pale nje tumeweka ndoo za maji ya kunawa, mlangoni usiingie ndani bila kunawa, takasa mikono na ukisha ingia kaa 'social distance' na uhakikishe unavaa barakoa na barakoa nzuri ni ile uliyoishona mwenyewe,"amesisitiza Dk. Chande huku akishangiliwa na waumini.


Mdau, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video Dk. Chande akiwapiga msasa waumini kuhusu mapambano dhidi ya janga la corona...

Imeandaliwa na Richard Mwaikenda 
Mhariri Blog ya Taifa ya CCM
0754264203

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages