LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 10, 2021

CCM,SERIKALI YAPIGA MARUFUKU MIRADI YA NGUVU ZA WANANCHI KUVUNJWA

 

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Magu, Mary Peter, akiwaeleza wajumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Magu jinsi mhandisi wa halmashauri ya wilaya hiyo, alivyoagiza vyumba vitatu vya madasara vilivyokuwa vikijengwa kwa nguvu za wananchi vivunjwe
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Magu, Zablon Makoye wa tatu utoka kushoto, akihoji jambo mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya hiyo ilipotembelea Shule ya Msingi Magu ili kujionea utekelezaji wa ilani ya uchaguzi.
Mkuu wa Wilaya ya Magu, Salum Kalli, akitoa maelezo kwa Wajumbe wa  Kamati ya Siasa ya Wilaya hiyo ilipotembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika sekta za elimu, afya, maji, na umeme. Picha na Baltazar Mashaka 
………………………………………………………………………….
NA BALTAZAR MASHAKA, MAGU
KAMATI ya Siasa ya CCM Wilaya ya Magu,imeiagiza Halmashauri ya Wilaya hiyo kukamilisha ujenzi wa madarasa matatu ya Shule ya Msingi Magu kwa fedha za mapato ya ndani ili kutowavunja nguvu wananchi.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Magu,Zabron Makoye, aliagiza jana kuwa kwa vile kwenye mradi huo kuna nguvu za wananchi halmashauri ihakikishe inakamilisha darasa lililobaki kwa fedha  za mapato ya ndani.

“Hii itatuletea shida na nguvu hizo za wananchi zitatuumiza maana unapovunja majengo unawakatisha tamaa, tafuteni fedha mkamilishe madarasa wakati  uchunguzi ukifanyika na atakayebainika kuhusika alitafuna fedha awajibike,”aliagiza Makoye na kuongeza;

“Mhandisi,changamoto za miradi inaonyesha unafanya kazi kwa mazoea bila kufika site hadi miradi inakamilika,safari nyingine hatutaki kupita na kuona madudu ya aina hiyo, hivyo jitathmini na ubadilike.”

Awali Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Magu, Mary Peter, aliieleza Kamati ya Siasa jana ilipotembelea na kukagua miradi ya maendeleo kuona utekelezaji wa ilani kuwa, wananchi walichangia kila mmoja sh.3,700  kwa ajili ya vyumba vitatu vya madasara na madawati ili kuwaondolea watoto changamoto ya kukaa chini.

Alieleza kuwa madarasa hayo matatu yaliyojengwa kwa michango ya wananchi, yalivunjwa kwa maagizo ya Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu kwa madai kuwa yalijengwa chini ya kiwango.

Mary alieleza zaidi kuwa  wananchi walianzisha ujenzi wa madarasa hayo matatu kwa nguvu zao,kabla ya Septemba 2020 kupokea fedha za EP4R sh.milioni 40 ambazo zimekamilisha madarasa mawili tu badala ya matatu.

Aliongeza kuwa mhandisi wa halmashauri, Mhandisi Msisdn Ok, kabla ya ujenzi wa madarasa hayo kuanza aliwashauri waweke nondo nne kila upande ili kuufanya msingi wake kuwa imara baada ya kukaa muda mrefu bila kujengwa lakini aligeuka na kuagiza yavunjwe.

“Cha  kushangaza mhandisi huyo alifika na tape akidai hawezi kuchezea kazi yake kwani miradi mikubwa ya aina hiyo inaweza kumwingiza kwenye matatizo akaagiza madarasa yavunjwe ingawa Mwenyekiti wa Halmashauri wa wakati huo, Elisha Hilal, aliagiza ujenzi uendelee ili kutowavunja moyo wananchi,”alisema Mary.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Magu, Salum Kalli, alisema serikali imepokea maelekezo ya kamati na kuagiza, ni marufuku kuvunja majengo yanayojengwa kwa nguvu za wananchi, pia mwalimu mkuu huyo wa shule asibughudhiwe na asihamishwe kituo cha kazi sababu amesimamia vizuri ilani.

Alisema binafsi aliumizwa sana kuvunjwa kwa madarasa hayo ambayo ndani yake kuna nguvu za wananchi,ili kutowaumiza watoto halmashauri ikae na kutafuta fedha ikamilishe jengo lililobaki wakati wakisubiri ukaguzi ufanyike wa matumizi ya fedha za EP4R.

Aidha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Magu, Simon Mpandalume, alisema hawakuridhishwa na fedha hizo sh. milioni 40 kujenga madarasa mawili tu na hivyo waliagiza ufanyike ukaguzi maalum (Special Auditing)kujiridhisha zilitumikaje.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages