LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 7, 2020

KIKAO CHA KWANZA CHA MKUTANO WA KWANZA WA BUNGE JIPYA KUFANYIKA NOVEMBA 10, 2020

 


TANGAZO LA KUITA WABUNGE DODOMA KUHUDHURIA MKUTANO WA KWANZA WA BUNGE LA KUMI NA MBILI

 

Kufuatia Tangazo la Rais la kuitisha Bunge lililotangazwa kwenye Gazeti la Serikali, Toleo Maalum (Special Supplement) la  tarehe 5 Novemba, 2020  (Tangazo Namba 942A) na kufuatia Tangazo nililolitoa kwenye Gazeti la Serikali Toleo Maalum  (Special Supplement)  la tarehe  5 Novemba, 2020 (Tangazo Namba 1763A)  kuhusu nafasi ya Spika kuwa wazi na utaratibu utakaotumika kujaza nafasi hiyo, pamoja na Gazeti la Serikali, Toleo Maalum  (Special Supplement) (Tangazo Namba 1764A) kuhusu nafasi ya Naibu Spika kuwa wazi na utaratibu utakaotumika kujaza nafasi hiyo na Kanuni za Uchaguzi wa Viongozi hao, Wabunge wote wanafahamishwa kwamba shughuli za usajili na taratibu nyingine za kiutawala zitafanyika Ofisi ya Bunge Dodoma kuanzia tarehe 7 – 9 Novemba, 2020. 

Hivyo basi, Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya kitafanyika tarehe 10 Novemba, 2020 kama ilivyotamkwa kwenye Tangazo la Rais. katika Mkutano huu wa kwanza wa Bunge la 12, shughuli zitakazofanyika ni pamoja na:

(a)             Kusomwa Tangazo la Rais la kuitisha Bunge

(b)             Uchaguzi wa Spika

(c)             Kiapo cha uaminifu kwa Wabunge wote

(d)             Kuthibitisha uteuzi wa Waziri Mkuu

(e)             Uchaguzi wa Naibu Spika

(f)       Ufunguzi rasmi wa Bunge Jipya utakaofanywa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tazania.

 

Aidha, inasisitizwa kwamba Wabunge Wateule wote wafike wakiwa na nyaraka zifuatazo:-

(a)             Hati ya Kuchaguliwa/Kuteuliwa kwa Mbunge;

(b)             Nakala ya kitambulisho cha Taifa;

(c)             Kadi ya Benki yenye Namba ya Akaunti ya Mbunge;

(d)             Cheti cha Ndoa kinachotambuliwa na Serikali (Kwa wenye Ndoa);

(e)             Cheti cha kuzaliwa cha Watoto wenye umri chini ya miaka 18 (Kwa wenye Watoto);

(f)                Vyeti vya Elimu/Taaluma;

(g)             Nakala ya Wasifu wa Mbunge (Curriculum Vitae);

(h)             Picha (Passport size) nakala 8.

 

 

Imetolewa na:  Katibu wa Bunge,

                         Ofisi ya Bunge,

                         DODOMA.

                       7 Novemba, 2020

1 comment:

  1. TUNALITAKIA BUNGE LETU KILA LA KHERI WANAPOANZA MAJUKUMU YAO YA KUTUWAKILISHA WATANZANIA. MWENYEEZI MUNGU AWABARIKI. AAAMIIIN.

    ReplyDelete

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages