LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Feb 7, 2020

NEC YAKAMILISHA UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA MIKOA 28. DAR, PWANI KUMALIZIA WIKI IJAYO


Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi jaji Semistocles Kaijage akizungumza na mkutano na wadau wa uchaguzi wa Mkoa wa Dar es Salaam wa kupeana taarifa juu ya zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani utakaoanza wiki ijayo. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA

Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Dkt.  Wilson Charles Mahera akizungumza na wadau wa uchaguzi wa Mkoa wa Dar es Salaam na kuwashauri wananchi kutumia haki yao ya kikatiba ya kushiriki katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka huu, 

Mkurugenzi wa Habari na Elimu ya Mpiga Kura wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Giveness Aswile akielezea katika mkutano huo kuhusu tofauti ya Elimu ya Uraia na Elimu ya Mpiga Kura.
 Baadhi ya viongozi wa siasa wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa NEC
 Baadhi ya viongozi wa Asasi za Kiraia, wenye urevu, vijana wanawake na wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam, wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Tume baada  ya mkutano huo kumalizika
 Katibu wa  Chama cha AFP Mkoa wa Dar es Salaam, Ndonge Said Ndonge akichangia mada wakati wa mkutano huo, ambapo aliitaka Tume kuanzia sasa watu wenye ulemavu waache kuwaita wenye makundi maalumu bali waitwe Makundi yenye Mahitaji Maalumu. Tume ililidhia ombi hilo.

Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji, Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam, Novaita Mrosso akiwasilisha mada katika mkutano huo wadau wa uchaguzi kuhusu sifa za kuwa raia wa Tanzania.
Baadhi ya wadau wa uchaguzi wakiwa katika mkutano huo
Baadhi ya Wadau wakisikiliza kwa makini wakati Mkurugenzi wa NEC, akiwasilisha mada kuhusu uhamasishaji wa katika uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura
Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake na Watoto wa Shirikisho la  Vyama  vya Watu wenye Ulemavu Tanzania, Nasiriya Nasir Ally akichangia mada wakati wa mkutano huo.
Katibu wa Chadema Mkoa wa Dar es Salaam, Waziri Muhuzi, akichangia mada wakati wa mkutano huo.
Baadhi ya viongozi wa Dini wakiwa na viongozi wa NEC
 
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Dkt.  Wilson Charles Mahera akizungumza na wanahabari kuhusu yaliyojiri kwenye mkutano huo.
                        Na Richard Mwaikenda
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), tayari imekamisha zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika ikoa 23 Tanzania Bara na mikoa mitano ya Tanzania Zanzibar.
Mikoa iliyobakia ni Morogoro katika baadhi ya halmashauri na mikoa ya  Dar es Salaam na Pwani ambayo unatarajiwa kufanyika kwa siku saba, kuanzia Februari 14 hadi 20 mwaka huu,

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano ulioikutanisha tume ya Taifa ya uchaguzi na wadau wa uchaguzi wa Mkoa wa Dar es Salaam Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini, Jaji Semistocles Kaijage amesema kuwa maandalizi kwa ajili ya zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura katika mikoa hiyo umekamilika na kuwataka wale wote wenye sifa kutumia haki yao ya kikatiba kwa kujiandikisha ili kuweza kushiriki katika katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka huu.


Amesema kuwa uboreshaji wa daftari la kudumu hautahusisha wapiga kura wote walioandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapiga kura mwaka 2015.

"Uboreshaji huu unawahusu wapiga kura wapya ambao wametimiza miaka 18 na wale ambao watatimiza umri wa miaka 18 siku ya uchaguzi mkuu mwaka huu." Ameeleza.

Aidha amesema kuwa kwa wale ambao wamehama kutoka maeneo yao ya awali na kuhamia maeneo mengine, wenye kadi zilizoharibika au kupotea na wale wanaotakiwa kuondolewa kwenye daftari kwa sababu za kufariki au kupoteza sifa watahusika katika maboresho hayo.


Vilevile amesema katika uboreshaji huo Kuna baadhi ya asasi za kiraia ambazo zimepewa vibali vya kutoa elimu kwa mpiga kura kwa ajili ya uboreshaji na kuwashauri wananchi kutumia nafasi hiyo kwa kujifunza kuhusu uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura na amezitaka asasi hizo ambazo zimepewa kibali na tume kutumia mwongozo wa utoaji wa elimu ya mpiga kura uliotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi juu ya uboreshaji wa daftari hilo.

Jaji Kaijage ametoa rai kwa wananchi wote kutunza kadi zao hadi siku ya uchaguzi na hata baada ya uchaguzi kwa kuwa moja ya changamoto kubwa iliyojitokeza katika baadhi ya maeneo yaliyokamilisha mchakato huo ni pamoja na upotevu wa kadi, kadi kuharibika na wananchi kushindwa kukumbuka majina yao hivyo kuchukua muda mrefu katika kutafuta majina yao kwa usahihi.
Pia amesema wananchi wajitokeza mapema na sio kusongamana misururu mirefu kwenye vituo vya kuandikisha wapiga siku za mwisho na kusema kuwa hilo litafanikiwa ikiwa wadau, tume na wananchi watashirikiana katika zoezi zima la uchaguzi.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Dkt. Wilson Charles Mahera amesema kuwa wananchi wenye sifa wajitokeze ili kutimiza haki zao za kiraia na kueleza kuwa Tume inatambua mchango wa wadau mbalimbali katika kuleta mabadiliko chanya na mwamko wa kimaendeleo katika jamii yetu.
Amesema kuwa Tume itaendelea kuzingatia Sheria na kanuni zake katika zoezi zima la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura na kuviomba vyama vya siasa na wadau wengine kuzingatia Sheria za uchaguzi, kanuni za uboreshaji na maelekezo kwa vyama vya siasa kuhusu zoezi la uboreshaji.


Mkutano huo umewakutanisha wajumbe wa Tume, viongozi wa vyama vya siasa, dini, Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam, wawakilishi wa watu wenye ulemavu, wanawake, vijana, asasi za kiraia na wahariri na waandishi wa habari.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages