LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 6, 2020

WAMEKUJA NA MBINU MPYA

Napenda kuleta mkasa huu, Nikiwa natafakari ujumbe huu hapa chini kwa siku hiyo ya Tarehe 03/01/2020 nilikuwa nasumbua kichwa na nililala nilipo amka Asubuhi tarehe 04/01/2020 niliona nipate kujuwa kulikoni,

Nilipiga simu kwa kutumia namba hizo chini nilizoambiwa katika Laini yako huwa unaweka pesa? nikajibu sijawahi kuweka na nikaambiwa umeshinda Milioni 5 na  ili kupata Pesa yako inabidi kuweka Elfu Ishirini na tano kwenye Simu yako ndani ya nusu Saa upate Bonus yako kwani ujumbe huu ni wajana na mlikuwa watu wanne na nikaulizwa

Nikwanini hujapiga toka jana nikajitetea nilikuwa safari ila kiukweli sikuwa safari, Basi nilikwenda na nguvu ya wasiwasi mpaka kwa wakala nikamwambia naomba unishauri kuisoma msg hii, aliisoma na kuniambia hawa ni matapeli 

Nikamwambia wakala tujaribu kuweka pesa, nikamtajia namba yangu ya Haloteli ili niweke pesa hiyo lakini chaajabu kila nikiitaja namba yangu inakuja jina lingine la kike na ndipo nilipiga huduma kwa wateja nikaulizia kwa mapana na marefu na wakaniambia niwatajie namba hizo nikaambiwa ni matapeli. hapa chini ni ujumbe niliotumiwa hiyo Tarehe 03.

No, Iliyotuma ujumbe huu ni 0621419235; Tarehe 03/01/2020 saa 09:31
Kutoka-Supar Halo
Hongera' Umeshinda Tsh Milioni Tano 50,000,000/Kutoka Halotel-Super HaloTupigie Simu No' 0625038240 kupata Bonus yako
Ahsante! 

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages