LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 2, 2020

SHIRIKA LAKUTETEA HAKI ZA WAFUNGWA (NDABARIZA) LATAKA MSAMAHA WA RAIS UTEKELEZWE HARAKA

  • Shirika la Kutetea Haki za Wafungwa nchini Burundi (NDABARIZA), limevitaka vyombo husika vya serikali kutekeleza agizo la Rais Pierre Nkurunziza la kuwaachilia huru wafungwa waliopewa msamaha na rais huyo.
Hii ni baada ya Rais Nkurunziza kutoa msamaha kwa wafungwa waliohukumiwa vifungo visivyozidi miaka mitano jela pamoja na wafungwa wajawazito, akina mama wanaonyonyesha na walemavu.
Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi
Hatua hiyo imetajwa kuwa itakayosaidia kupunguza msongamano wa sasa katika jela zote za Burundi. Taarifa zinasema kuwa, jela kuu ya Mbimba ya mjini Bujumbura, ilijengwa ikiwa na uwezo wa kuwahifadhi wafungwa 800 pekee, lakini kwa sasa lina zaidi ya wafungwa 4000.
Jiunge na mwandishi wetu wa mjini Bujumbura, Hamida Issa kwa kubonyeza alama ya sauti pale juu………………./

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages