• Home
  • About CCM's Official Blog
  • Contact/Mawasiliano

CCM Blog
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • KIJAMII
    • SIASA
    • BIASHARA
    • UCHUMI
    • MICHEZO
    • BURUDANI
    • MAKALA
    • MAGAZETI
  • LATEST HEADLINES👉

    Your Ad Spot

    Jan 8, 2020

    Home Elimu featured PROF. MUHONGO AZINDUA SHULE BINAFSI YA AGAPE YA MZAWA WA KIJIJI CHA BUKIMA, KAYOLE MUSOMA VIJIJINI

    PROF. MUHONGO AZINDUA SHULE BINAFSI YA AGAPE YA MZAWA WA KIJIJI CHA BUKIMA, KAYOLE MUSOMA VIJIJINI

    Richard Mwaikenda January 08, 2020 ,Elimu ,featured
    Wanafunzi, Walimu, Wazazi, Viongozi wa Serikali na Chama (CCM) wamehudhuria SHEREHE za UZINDUZI wa AGAPE Primary School zilizofanyila Jumanne, 7.1.2020 Kijijini Bukima.
    KIONGOZI na MMLIKI wa Shule hiyo, Ndugu ANDREW KAYOLE (32yr), mhitimu wa UDOM, Shahada ya Biashara  Bc(HRM) amesema Shule hiyo ilisajiliwa rasmi tarehe 21.6.2017 na tayari WAHITIMU wa kwanza wamemaliza Darasa la 7 (Std 7) Mwaka jana (2019) wakiwa wa KWANZA kwa Wilaya ya Musoma katika kundi lao. 
    Wanafunzi wote walifaulu (A&B). Shule inafundisha kwa lugha ya KIINGEREZA na Mwakani lugha ya KIFARANSA itaanza kufundishwa Shuleni hapo.
    MGENI RASMI, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo amesema kwamba kuwepo kwa Shule Binafsi (Private Schools) Jimboni mwao ni muhimu sana kwa UIMARIKAJI wa UBORA wa ELIMU kupitia USHINDANI KITAALUMA kwa Shule zote za Msingi zilizoko Jimboni humo (Shule 3 za Binafsi na 111 za Serikali).
    Mbunge huyo amekuwa AKICHANGIA MAENDELEO ya Shule za Msingi na Sekondari za Serikali na Binafsi bila UBAGUZI wo wote. 
    Aliwakumbusha WAGENI waalikwa kwamba Vyuo Vikuu bora Duniani vimo vya Binafsi (Private Universities) kama vile Harvard (USA),  MIT (USA), Yale (USA) Caltech (USA), na vilevile vimo vya umma (Public Universities) kama vile Oxford (UK) na Cambridge (UK).
    Mbunge huyo amechangia box 10 za VITABU vya Maktaba ya Shule hiyo. Vilevile, amechangia SARUJI MIFUKO 50 kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la TEHAMA. Ametoa ahadi ya kuchangia COMPUTER 1 na PRINTER 1 mara Jengo hilo litakapokamilika na kuanza kutumika.
    Wakati akizindua AGAPE Primary School na kuweka Jiwe la Msingi la Jengo la TEHAMA la Shule hiyo, Mbunge huyo AMEMWOMBA MWANZILISHI wa Shule hiyo aendelee kuipanua hadi kuanza kutoa MASOMO ya SEKONDARI.
    WAZALIWA KUWEKEZA VIJIJINI MWAO
    MMILIKI (Ndugu ANDREW KAYOLE) wa Agape Primary School ni KIJANA (32yr) ALIYETHUBUTU na KUFANIKIWA kuwekeza Kijiji mwao. 
     Mbunge wa Jimbo AMEMPONGEZA SANA na kusema JIMBO LINAJIVUNIA kuwa na WAWEKEZAJI wa aina hiyo – TUJIFUNZE KWAKE na TUWEKEZE Vijijini kwetu!
     MGENI RASMI, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo (kushoto)  na mmiliki wa shule hiyo,  Andrew Kayole (wa pili kulia) pamoja na viongozi wa mbalimbali wakipiga makofi ikiwa ni ishara ya kufurahia baada ya  kuzindua rasmi shule hiyo.
     Profesa Muhongo akiangalia jiwe la msingi baada ya kuizindua rasmi shule hiyo.
     Profesa Muhongo akiwa na viongozi wengine pamoja baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo
     Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof. Muhongo (kulia) akizungumza jambo na viongozi pamoja na mmiliki wa shule hiyo, Kayole.
    Prof. MUHONGO AKIWA NA BAADHI YA VIONGOZI PAMOJA NA BAADHI YA WANAFUNZI BAADA YA KUZINDUA SHULE HIYO YA AGAPE.



  • Share
  • Tweet
  • Share



    • Email

    Post navigation

    ← HAYUPO MWANAFUNZI WA KIDATO CHA…


    Tafuta katika Tovuti hii

    Machapisho ya Karibuni

    • MZALIWA WA KIJIJI CHA BUKIMA AANZISHA SHULE YA MSINGI KIJIJINI MWAO – YAZINDULIWA RASMI LEO January 8, 2020
    • HAYUPO MWANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA 2020 (wamechaguliwa 3,502) ATAKAYEBAKI NYUMBANI January 6, 2020
    • MICHEZO JIMBONI – UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM YA 2015-2020 January 1, 2020
    • MASHINDANO YA KUPIGA KASIA 2019 (THE ANNUAL BOAT RACE) December 29, 2019
    • SIKUKUU YA KRISMASI KIJIJINI NYASAUNGU – WANAKIJIJI WASISITIZA SEKONDARI YAO KUFUNGULIWA MWAKANI (2020) December 27, 2019

    Kalenda

    January 2020
    M T W T F S S
    « Dec
    12345
    6789101112
    13141516171819
    20212223242526
    2728293031
    Tags Elimu# featured#
    Share This
    Author Image

    About Richard Mwaikenda

    featured
    By Blog CCM Blog Richard Mwaikenda - January 08, 2020
    Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
    Tags Elimu, featured

    No comments:

    Post a Comment

    Tupia Comments👇

    Newer Post Older Post Home
    Subscribe to: Post Comments (Atom)

    Post Top Ad

    Your Ad Spot

    KWAKO MTANZANIA

    KWAKO MTANZANIA

    ILANI YA UCHAGUZI YA CHAMA CHA MAPINDUZI YA 2025/30

    ILANI YA UCHAGUZI YA CHAMA CHA MAPINDUZI YA 2025/30

    VIONGOZI WAKUU WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)

    VIONGOZI WAKUU WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
    Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan

    MAKAMU MWENYEKITI WA CCM ZANZIBAR

    MAKAMU MWENYEKITI WA CCM ZANZIBAR
    Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar Dk. Hussein Mwinyi

    MAKAMU MWENYEKITI WA CCM, BARA

    MAKAMU MWENYEKITI WA CCM, BARA
    Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Steven Wasira

    KATIBU MKUU WA CCM

    KATIBU MKUU WA CCM
    Balozi Dk. Asha-Rose Migiro

    Chagua Lugha/Translate Language👇





    Tafuta (Search) hapa👇

    CCM Blog. Powered by Blogger.

    Pages

    • Home


    Idadi ya wanaosoma CCM Blog

    Tuma Ujumbe hapa

    Name

    Email *

    Message *

    This Blog Designed and Developed By Bashir Nkoromo | Bashir Nkoromo | Property of Chama Cha Mapinduzi