LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 12, 2019

KITABU CHA UJASIRI WA PEKEE WA RAIS MAGUFULI KUZINDULIWA DESEMBA, 2019



"Finest Valor" Ujasiri wa Pekee" Simulizi ya Kuibuka kwa Rais John Pombe Magufuli.

 KITABU cha Mafanikio ya Rais Dr.John Pombe Magufuli, kuanzia mchakato wa kumpata kama mgombea, kampeni ya Urais 2015, kuapishwa Novem Ba 5 2015, sera na mipango yake. 

Ujasiri wa kusimamia rasilimali za nchi, kufufua shirika la ndege, kujenga misingi ya uzalendo, sera ya mambo ya nje na kufanikiwa kupambana na rushwa na ufisadi kwa kiwango cha juu.

Kitabu hicho kimeandikwa na Novatus Joseph Igosha Mwanasheria Wizara ya katiba na sheria na kinatarajiwa kuzinduliwa Disemba 2019.

Kimehaririwa na Spika mstaafu wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Pius Msekwa, kitabu hicho kwa sasa kimepitishwa katika kampuni ya Afrika kusini inaitwa Reach Publishers.

Kitabu hicho kinalengo la kujenga uzalendo kwa kuonesha ujasiri wa serikali ya Rais Magufuli katika kuwatumikia wananchi kwa kufanya maamuzi kijasiri katika kusimamia rasilimali za nchi, kupambana na rushwa na ufisadi kizalendo.

 Ila pia kutambulisha upekee wa serikali hii katika kujenga uchumi wa kati na wa viwanda kwa siku zijazo.

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages