LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 29, 2019

WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA TANO WAPEWA WIKI MBILI KUBADILI TAHASUSI

Serikali imetoa fursa ya wiki mbili kwa wanafunzi waliofaulu kujiunga na kidato cha tano kufanya mabadiliko ya machanganuo ya tahasusi na kozi mbalimbali walizochagua kwenye fomu ya F4 Selform.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Selemani Jafo wakati akiongea na waandishi wa habari leo ofisini kwake amesema kuwa wiki hizo mbili zitaanza mwezi wa Aprili Mosi hadi 14 mwaka huu.

Aidha Waziri Jafo amesema kuwa fursa hiyo ni ya kwanza kutolewa mwaka huu na ni mara ya kwanza ambayo itawawezesha wanafunzi kurekebisha mchanganuo huo kulingana na ufaulu walioupata katika matokeo ya kidato cha nne ya mwaka 2018 yaliyotolewa na Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)

Waziri Jafo amesema kuwa  hali hiyo inatokana na baadhi ya wanafunzi ambao hawakujaza vizuri tahasusi zao kutokana na kutokuwa na uhakika wa ufaulu.

”Ofisi yangu inatoa fursa hii kwa wahitimu kubadili mchanganuo ili kutoa mwanya zaidi kwa wanafunzi kusoma fani au tahasusi itakayomwandaa kuwa na utaalamu fulani kwenye maisha yake ya baadae kwa nafasi yake ambayo anatamani yeye mwenyewe au kwa kushauriwa na wazazi au walezi wake ”amesema Jafo

Hata hivyo amesema Ofisi yake tayari imeshakamilisha zoezi la awali la kuingiza taarifa zilizo kwenye Selform za wanafunzi kwenye kanzidata ya Tamisemi na mabadiliko hayo yatakayofanyika kwa njia ya mtandao yakikamilika kanzidata hiyo itatumika kuwachagua na kuwapangia kidato cha tano na kozi za vyuo.

”Kwa mwanafunzi yeyote atakayekuwa hajabadilisha taarifa zake mpaka muda kuisha Ofisi yake itaamini kuwa wanafunzi huyo ameridhika na machaguo yake ya tahasusi aliyoyafanya hapo awali alipokuwa shuleni” amesisitiza Jafo

1 comment:

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages