CCM Blog, Kariakoo
Mkuu
wa Wilaya ya Ilala, Mh. Edward Mpogolo, ameiagiza Halmashauri ya Jiji
la Dar es Salaam, Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) na
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kuanza
mara moja kuzibua mitaro, mifereji na chemba za kupitisha maji taka
maeneo ya Kariakoo.
Ametoa agizo hilo alishirikiana na viongozi na wananchi kufanya usafi leo Jumamosi, Septemba 12, 2026, ikiwa ni utekelezaji wa kampeni endelevu ya usafi inayofanyika kila Jumamosi.
Ufanyaji
usafi huo ulioongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Ndugu
Abdul Muhite, akishirikiana na Wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Mkoa na
Wilaya.
Viongozi wengine walioshiriki ni pamoja Diwani wa
Kariakoo Haji Manara, Diwani wa Jangwani Mohamed Zaidi, Katibu Tawala
wa Wilaya ya Ilala Charangwa Selemani,
Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Elihuru Mabelya na Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko Kariakoo.
Wengine
ni Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Rajabu Amiry, akiwa
ameambatana na wasanii wa filamu Tanzania, pamoja na Kampuni za Usafi za
SATEK, KAJENJERE, TIRIMA na WEJISA, Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo
(JWK) na KAWASSO.
Mhe. Mpogolo amesema mitaro na mifereji
iliyoziba kutokana na taka inaweza kusababisha maji kushindwa kupita
wakati wa mvua na hivyo kuhatarisha usalama wa wananchi, biashara na
miundombinu.
“Natoa agizo kwa Halmashauri ya Jiji la Dar es
Salaam, TARURA na DAWASA, kuanza mara moja kazi ya kuzibua mitaro,
mifereji na chemba za maji pamoja na kuondoa takataka zilizoziba
mifereji hiyo. Takataka hizi zinasababisha mifereji kushindwa kufanya
kazi ipasavyo hivyo kuweza kusababisha madhara makubwa wakati wa mvua.”
amesema Mh. Mpogolo.
Amesema Mamlaka za hali ya hewa zimeendelea
kutoa tahadhari kuhusu uwezekano wa kuwepo kwa mvua kubwa, hivyo ni
muhimu maandalizi yakafanyika mapema kwa kuhakikisha mitaro na mifereji
inakuwa wazi na inafanya kazi ipasavyo.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Rdward Mpogolo akkitoa agizo hilo.














No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇