LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 11, 2026

CDE MKANDAWIRE NA CDE MTUA WATOA SALAMU ZA POLE KWA MWENYEKITI WA CCM RAIS DK. SAMIA, NI KWA NIABA WA MAKATIBU WA CCM WA MIKOA YOTE

 

Katibu wa Chana Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Cde Stanley Mkandawire na Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Cde Omar Mtua, juzi walifika kutoa salamu za pole kwa Mwenyekiti wa CCM) Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kufuatia kifo cha mwenza wake Marehemu Hafidh Ameir Hassan.

Cde Mkandawire na Cde Mtua wametia salamu hizo kwa niaba ya Makatibu wa CCM wa Mikoa yote ya Tanzania.

Wakiwasilisha salam hizo,  wameeleza masikitiko yao na kumuombea Mwenyekiti Dk. Samia na familia ndugu na marafiki Mungu awape nyoyo za subra katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.

“Tunamuomba Mwenyezi Mungu awape subra, nguvu na moyo wa uvumilivu katika kipindi hiki cha majonzi. Mwenyezi Mungu amsamehe marehemu Hafidh Ameir Hassan, amrehemu na amlaze mahali pema peponi. Amina.”

INNA LILLAHI WA INNA ILAYHI RAJI’UN

Katibu wa Chana Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Cde Stanley Mkandawire na Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Cde Omar Mtua (Kulia), wakitoa salamu za pole juzi, kwa Mwenyekiti wa CCM) Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kufuatia kifo cha mwenza wake Marehemu Hafidh Ameir Hassan.

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages