Mwenyekiti wa Jumuiya ya W
azazi Taifa Ndg. Fadhili Maganya ameridhishwa na utekelezaji wa mradi wa maji unatekelezwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Kibiti.
Amesema mradi huo ni mkombozi mkubwa katika kuwahudumia kwa kiasi kikubwa wananchi na kwamba upatikanaji wa maji safi na salama utawapunguzia adha wanannchi kwa kutembea umbali mrefu.
Hayo ameyabainisha wakati wa ziara yake ya kikazi katika Wilaya ya Kibiti yenye lengo la kuweza kuimarisha chama, kuangalia utekelezaji wa Ilani pamoja na jumuiya zake zote sambamba na kutembelea na kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo, ikiwemo sekta ya elimu pamoja na sekta ya maji.
Mwenyekiti huyo amesisitiza kwa uongozi wa Ruwasa kuendelea kuhakikisha wanaweka ulinzi wa kutosha katika mradi huo ambapo amesema chanzo hicho ni muhimu sana kwani ndio tegemezi kubwa la wananchi wa Wilaya ya Kibiti katika suala zima la upatikanaji wa maji safi na salama na kuwahimiza kutunza chanzo cha maji hayo pamoja miundombinu iliyopo.
"Nipende kuchukua nafasi hii kuwapongeza kwa dhati uongozi mzima wa Ruwasa kwa kutekeleza mradi huo wa maji ambao utakuwa ni msaada mkubwa kwa wananchi wa Wilaya ya Kibiti,"amebainisha Mwenyekiti.
Akizungumza katika mkutano wa ndani na wanachama wa chama hicho amewaomba viongozi kuhakikisha kwamba wanatekeleza ilani ya chama kwa vitendo ikiwemo suala la kusimamia fursa za mikopo ya asilimia 10 ambayo inatolewa na Halmashauri.
Pia amewaagiza viongozi wa chama pamoja na madiwani kuhakikisha wanasimamia fedha zinazotolewa kwa ajili ya miradi ya maendeleo.
Meneja huyo amebainisha kwamba lengo kubwa la ukarabati wa mradi huo ni kwa ajili ya kuweza kutatua changamoto ya maji ambazo zinawakabiliwa wananchi wa Wilaya ya Kibiti na kuunga juhudi za serikali ya awamu ya sita katika kuhakikisha ina mtua mama ndoo kichwani
.
Amebainisha ukarabati wa.mradi wa maji Kibiti mjini umetekelezwa kwa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 312 ambazo fedha hizo zimetolewa na serikali kuu kupitia mfuko wa maji wa fedha Kitaifa (NWF) na kwamba utakuwa ni mkombozi mkubwa katika kutatua changamoto hizo zilizokuwa zinawakabili wananchi.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amempongeza kwa dhati Mwenyekiti wa wazazi Taifa kwa kutekeleza ilani ys chama kwa vitendo ikiwemo suala la kufanya ziara ya kikazi ambayo imekuwa na mafanikio makubwa kutokana na kuweza kukutana na viongozi wa serikali, taasisi wezeshi pamoja na chama.
Kanali Kolombo amebainisha kwamba hali ya amani na utulivu katika Wilaya ya Kibiti inaendelea vizuri na kwamba katika utekelezaji wa ilani wameweza kupokea kiasi cha shilingi milioni 528 kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Mchukwi ambapo pia wamepokeai kisi cghha shilingi milioni 700 kwa lengo la kuboresha miundombinu ya barabara hususan zinazowenda maeneo ya Delta na sehemu nyingine.
No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇