Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Ado Shaibu, amezionya Halmashauri za wilaya nchini kuacha tabia ya kudharau na kupuuza hoja na maelekezo ya kamati hiyo na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Ametoa onyo hilo alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari baada ya kamati hiyo kufanya kikao na viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Same jijini Dodoma Agosti 20, 2026.
"Ifahamike kwamba kamati yake inafanya kazi kwa niaba ya bunge, kuidharau kamati hiyo ni swa na kulidharau bunge kitu ambacho hakikubaliki hata kidogo,"amesema Shaibu.
Wabunge ambao ni wajumbe wa kamati hiyo wakiwa katika kikao hicho.
Mmoja wa viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same akijibu hoja.
https://youtu.be/F0h0FaJ9a1s

No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇