LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 1, 2026

VIJANA ACHENI KUTUMIKA, DUMISHENI AMANI-MRAMBA

Katibu wa siasa,uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. David Mramba amewaasa wananchi hususan  vijana kuwa wazalendo na nchi yao na  kuachana kabisa  na vitendo  vya  kutumika  kwa maslahi ya makundi ya watu wengine na badala  yake kuhakikisha wanaweka misingi ya kuwa walinzi na kudumisha amani.


Dkt. Mramba ameyabainisha hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari  Ofisini kwake kuhusiana na masuala  ya wananchi kuwa na jukumu la kulinda  amani katika maeneo yao na kuwahimiza wanapaswa kuzingatia katiba na sheria  na kutojiingiza katika vitendo ambavyo vinaweza kuhatarisha  usalama wa maisha yao
.
"Suala la amani ni jambo  la muhimu sana kati yetu hivyo niwasihi wananchi  wote wa Mkoa wa Pwani  msikubali hata kidogo  kuwashawishi kufanya vitendo vyovyote ambavyo vinaweza kuhatarisha usalama   wa maisha , ikiwemo mali pamoja na uchumi wetu kwani amani ni msingi mkubwa wa maendeleo,"amebainisha Dkt. Mramba .

Aidha Katibu huyo amewahimiza wazazi na walezi kuhakikisha wanawalinda  watoto wao na kwamba kila kijana anapaswa kufikiria mustakabali wake ikiwa pamoja na kuweza kulinda amani na  kuitunza katika  maeneo yao wanayoishi.

Pia Katibu  huyo amebainisha kwamba Mkoa wa Pwani umebarikiwa  kuwa na lango muhimu la uchumi wa Taifa wakiwemo wakulima,wafugaji ,wavuvi, na wafanyabiashara na wawekezaji kwa hiyo kunahitajika kuwa na mazingira mazuri yenye amani na utulivu.

Mramba pia amewaomba wananchi  wote wa Mkoa wa Pwani kuendelea kuwa walinzi  wa amani na kwamba wanatakiwa kushirikiana  bega kwa bega  na vyombo vya dola  katika kulinda  usalama na kuendelea kujenga Tanzania yenye  umoja  na mshikamano  na maendeleo.

Aidha Katibu  amebainisha kwamba chama cha mapinduzi (CCM)  Mkoa wa Pwani kinampomgeza na kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kudumisha hali ya amani na utulivu katika Taifa la Tanzania.
                                                  
                                                      

 

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages