KAIMU Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Mhandisi Ephatar Mlavi, ametangaza miradi mikubwa ya maendeleo ya barabara pamoja na fursa mbalimbali kwa vijana kwa mwaka wa fedha 2025/2026.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mhandisi Mlavi amesema kuwa taasisi hiyo imejipanga kuendelea kuboresha miundombinu ya barabara nchini kwa kuzingatia ubora na uimara, sambamba na kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.
Ameeleza kuwa miongoni mwa vipaumbele ni utekelezaji wa miradi ya dharura ya kurejesha mawasiliano katika maeneo yaliyoathirika, pamoja na ujenzi wa miundombinu imara itakayoweza kuhimili athari za mazingira.
"Miradi hiyo inatekelezwa kupitia mpango wa Contingency Emergency Response Component (CERC)," Amesema Mhandisi Mlavi.
Kwa upande wa ukuaji wa miji, Mlavi amebainisha kuwa TANROADS itaendelea na miradi ya kupunguza msongamano wa magari katika miji mikubwa ikiwemo ujenzi na uboreshaji wa mfumo wa Dar Rapid Transit (BRT) katika jiji la Dar es Salaam, pamoja na ujenzi wa barabara za mzunguko na bypass katika miji mbalimbali kama Dodoma, Arusha na Songea.
Amesisitiza kuwa miradi hiyo pia inalenga kufungua fursa za ajira kwa vijana, hususan katika sekta ya ujenzi, usimamizi wa miradi na huduma za usafirishaji.

No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇